Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Kenya afariki dunia

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya Wafula Chebukati amefariki Dunia katika hospitali ya Nairobi akiwa na umri wa miaka 62.

Chebukati ambaye alisimamia uchaguzi wa rais wa mwaka wa 2017 na uchaguzi wa wa 2022 ambao uligawanya tume ya uchaguzi alishika hatamu mnamo Januari 2017 kufuatia kuondolewa kwa Ahmed Issack Hassan na makamishna wenzake na kuhitimisha utumishi wake wa miaka 6 kwenye Tume hiyo mnamo Januari 2023.

“Nimepokea habari ya kufariki kwa mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya zamani, Wafula Chebukati kwa masikitiko makubwa. Chebukati alikuwa kiongozi mwenye kanuni na mwenye bidii ambaye aliitumikia taifa kwa uadilifu,” ameandika Rais wa Kenya, William Ruto kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii na kuongeza:

“Kifo chake ni pigo kubwa kwa nchi yetu. Mawazo na sala zetu ziko na familia yake na marafiki wakati huu mgumu. Pumzika kwa amani,”.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...