Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Kenya afariki dunia

Na Mwandishi Wetu

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya Wafula Chebukati amefariki Dunia katika hospitali ya Nairobi akiwa na umri wa miaka 62.

Chebukati ambaye alisimamia uchaguzi wa rais wa mwaka wa 2017 na uchaguzi wa wa 2022 ambao uligawanya tume ya uchaguzi alishika hatamu mnamo Januari 2017 kufuatia kuondolewa kwa Ahmed Issack Hassan na makamishna wenzake na kuhitimisha utumishi wake wa miaka 6 kwenye Tume hiyo mnamo Januari 2023.

“Nimepokea habari ya kufariki kwa mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya zamani, Wafula Chebukati kwa masikitiko makubwa. Chebukati alikuwa kiongozi mwenye kanuni na mwenye bidii ambaye aliitumikia taifa kwa uadilifu,” ameandika Rais wa Kenya, William Ruto kwenye ukurasa wake wa mitandao ya kijamii na kuongeza:

“Kifo chake ni pigo kubwa kwa nchi yetu. Mawazo na sala zetu ziko na familia yake na marafiki wakati huu mgumu. Pumzika kwa amani,”.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...