WHO yatangaza tarehe ya uchaguzi wa kupatikana mrithi wa Ndugulile

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa Mkurugenzi mpya wa Kanda ya Afrika atachaguliwa Mei mwaka huu.

Uteuzi huo unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi mteule wa WHO Kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile aliyefariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Kutokana na kifo chake, WHO imeamua Mataifa yateue tena wagombea, huku tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ikiwa Februari 28, mwaka huu.

Dkt. Tedros Ghebreyesus ametangaza kuwa mchakato wa kura utafanyika Mei 8, 2025 na jina la kiongozi mpya litapitishwa rasmi Agosti 2025.

Aidha WHO imemteua Dkt. Chikwe Ihekweazu kama Kaimu Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika.

spot_img

Latest articles

MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba...

DAWASA YAWASHIRIKISHA WAFANYABIASHARA UDHIBITI UPOTEVU WA MAJI

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 220 IGANJO–SAZA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA UCHIMBAJI WA MADINI – MHE. SALOME

📌 Ashuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza,...

More like this

MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba...

DAWASA YAWASHIRIKISHA WAFANYABIASHARA UDHIBITI UPOTEVU WA MAJI

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...