Chalamila awaalika wakazi wa Dar kujitokeza kwa wingi uzinduzi wa Kituo cha biashara cha EACLC

Na Tatu Mohamed

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewaalika Watanzania na wakazi wa Jiji hilo kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa Kituo Kikubwa cha Biashara na Usafirishaji (EACLC), utaofanyika Agosti 1, 2025 katika eneo la zamani la Stendi Kuu ya Ubungo.

Chalamila amesema uzinduzi huo utafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye atakuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ya kihistoria.

“Nitoe wito kwa wananchi wote, wafanyabiashara waliokwisha chukua maduka, wale wanaotarajia kuchukua, na wote wanaopenda maendeleo ya biashara nchini, wafike kushuhudia tukio hili muhimu. Ni uzinduzi wa kituo ambacho kitabadilisha taswira ya biashara si tu Tanzania, bali Afrika Mashariki kwa ujumla,” amesema Chalamila.

Ameeleza kuwa kituo hicho kikubwa kimejengwa katika eneo ambalo awali lilikuwa Stendi ya Ubungo, baada ya serikali kuhamishia shughuli hizo Mbezi.

“Katika eneo hilo, serikali kupitia Mamlaka ya Uwekezaji kwa kushirikiana na wawekezaji kutoka China, imefanikisha ujenzi wa kituo cha kisasa cha kibiashara.

“EACLC ni mradi wa kimkakati uliogharimu zaidi ya dola milioni 100. Kina maduka zaidi ya 2,000, maghala ya kisasa, sehemu za ofisi, maegesho ya magari, na huduma nyingi nyingine za kibiashara zinazopatikana kwa kukodishwa kwa Watanzania na hata wageni kutoka nje,” alifafanua.

Amesema Kituo hicho kilianza kujengwa Mei 2023 na sasa ujenzi wake umekamilika.

Chalamila amesema ujenzi huo ni ishara ya dhamira ya serikali kuendeleza mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, huku akisisitiza kuwa uwekezaji huo haujachukua nafasi ya wafanyabiashara wazawa bali ni mfumo wa ubia unaowanufaisha wote.

Ametoa wito kwa wawekezaji wengine kufika kwenye Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi kupata taarifa sahihi za jinsi ya kuwekeza nchini.

spot_img

Latest articles

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...

Serikali yawataka wakuu taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya kazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewataka wakuu wa taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya...

More like this

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...