Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu

JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na mkazi wa Kata ya Somanga wilayani Kilwa, kwa tuhuma za kumuua kwa kumkata na panga mke wake wa zamani, Aisha Mkimbizi (41), mjasiriamali wa biashara ya samaki.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, ACP John Imori,  mtuhumiwa alitekeleza tukio hilo baada ya kuamini taarifa alizopewa na mganga wa kienyeji kuwa marehemu alikuwa akimloga na kusababisha kuishiwa nguvu za kiume.

Amesema tukio hilo lilitokea Aprili 26, saa 12 asubuhi, wakati marehemu akitoka Somanga kuelekea baharini kwa shughuli zake za biashara ya samaki. Inadaiwa mtuhumiwa alimvamia na kumkata kwa mapanga, hali iliyosababisha kifo chake akiwa njiani kupelekwa kituo cha afya.

Jeshi la Polisi linamshikilia pia mganga wa kienyeji, Haji Said Nguvunze (46), mkazi wa Somanga, ambaye amekiri kumweleza mtuhumiwa kuwa mke wake waliyetalikiana ndiye anayemloga.

Polisi wametoa wito kwa wananchi kuachana na imani za kishirikina na kuamini ramli chonganishi zinazosababisha madhara kwa watu wasio na hatia.

spot_img

Latest articles

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

Watu 37 washikiliwa kwa makosa ya mtandao

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 37 kwa...

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

More like this

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

Watu 37 washikiliwa kwa makosa ya mtandao

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 37 kwa...