Prof. Kabudi: Anayefanya kazi bila ‘Press Card’ anavunja Sheria

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari.

Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika, Julai 14, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Phillip Mpango jijini Arusha.

Amesema Press Card aliyopewa siyo kwa hisani bali ni kutokana na kukidhi vigezo, akiwa amewasilisha vyeti vya taaluma ya Uandishi wa Habari kwenye mfumo wa Bodi, huku akiwasisitiza Waandishi wengine kujisajili katika mfumo wa TAI-HABARI.

Waziri Kabudi amemuhoji Katibu Mtendaji Mstaafu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) ambao ni wenyeji wa Mkutano huo, Kajubi Mukajanga kama ameshajisajili na kupata Press Card, ambapo amekiri kuwa bado lakini atafanya hivyo siku chache zijazo nyaraka zake zikikamilika.

Mkutano wa Mabaraza la Habari Afrika unafanyika kwa mwaka wa pili nchini Tanzania ukitanguliwa na Mkutano wa kwanza uliofanyika Mwaka jana nchini Afrika Kusini.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...