Mashambulizi Israel| Watanzania wawili hawajulikani walipo

*Ni wanafunzi, Ubalozi waeleza

Yerusalemu, Israel

Ubalozi wa Tanzania nchini Israel unasema kuwa hauna mawasiliano naWatanzania wawili ambao wanakaa eneo la kusini ambalo limeshuhudia mapambano baina ya wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas na jeshi la Israeli.

Balozi wa Tanzania nchini Israel, Alex Kallua amelielezwa Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC) mapema leo Oktoba 9, kuwa mpaka leo asubuhi, ubalozi huo umekuwa na mawasiliano na Watanzania takribani 350 waliopo nchini humo kasoro wanafunzi hao wawili.

Balozi Kallua amesema: ”Tunaendelea kuwafuatilia Watanzania wawili ambao ni wanafunzi waliokuwa wanafanya mafunzo kwa vitendo ‘internship’ kusini mwa nchi hiyo. Tunafanya jitihada za kuwapata kwanza ili kufahamu walipo na hali zao.…wanafunzi wengine takribani 260 kati ya Watanzania zaidi ya 350 wako salama katika maeneo mbalimbali nchini humo na wamekuwa na mawasiliano na ubalozi,” amesema Balozi huyo.

Sambamba na hayo, balozi huyo amesema kuwa wanaendelea kufuatilia hali ya usalama nchini humo ili kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa salama.

”Tunafuatilia kwa karibu, na tunaendelea kupata taarifa kutoka Mamlaka za Israel kuhusu hali ilivyo. Tunaendelea kufuatilia na kuwaeleza waliopo hali ilivyo,” amesema balozi huyo.

spot_img

Latest articles

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Mradi wa Taza kufungua Soko jipya la biashara ya umeme Afrika

Na Mwandishi Wetu, Mbeya IMEELEZWA kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya...

More like this

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...