Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu

MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa la kukataa bao halali la Simba wakati wa mchezo na Yanga ulichezwa Machi Mosi, 2026 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Ligi iliyotolewa leo baada ya kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kilichokaa Machi 4, 2026 kupitia mwenendo wa matukio mbalimbali ya ligi, mwamuzi huyo ambaye alikuwa msaidizi namba moja katika mchezo huo alishindwa kutafsiri vyema sheria za miguu.

Taarifa ya wataalamu wa kutafsiri sheria za soka baada  kufanyia tathmini ya video ya tukio imebaini kuwa hakukuwa na kola lolote kabla ya kufungwa kwa bao hilo.

Naye mwamuzi msaidizi namba mbili wa mchezo huo, Hamdan Said kutoka Mtwara amefungiwa miezi mitatu kwa kosa la kusimamisha mchezo katika dakika ya 61 ya mchezo, akisimamisha shambulizi Yanga dhidi ya Simba kwa kuashiria kimakosa kuwa mchezaji Prince Dube alikuwa katika eneo la kuotea.

Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 42:1(1.8) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa waamuzi.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...