Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi

MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex wanatarajia kupanda ulingoni Machi 21, 2026 kusaka heshima ya Tanzania One katika pambano litakalopigwa Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam.

Siku hiyo imeandaliwa maalumu kwa ajili ya kusherehekea maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani, kutakuwa na mapambano mengi yatakayowakutanisha mabondia mbalimbali kutoka mikoa tofauti.

Akizungumzia maandalizi ya pambano hilo lililopewa jina la Punch kwa Heshima, Halima amesema yeye ni bondia mkubwa, amecheza na mabondia wengi wakubwa hivyo hana hofu na mpinzani wake.

“Huwa sina show mbovu, mabondia wa kike Tanzania wananielewa vizuri, nimepigana nchi kibao nimekutanza na changamoto nyingi nje ya nchi na Watanzania wanaijua kazi yangu. Sara Alex anajua anakwenda kucheza na bondia mkubwa,” ametamba.

Amejinasibu kuwa katika uzoefu wake wa masumbwi amecheza na mabondia wakali wa nje ya nchi na amewahi kutwaa ubingwa wa WBF nchini Ujerumani, ameshinda pambano Afrika Kusini, hivyo hakuna ninachomzuia kupiga mpinzani wake.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...