Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Catherine Fito, mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Umanda Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, amejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu, huku chanzo cha kifo hicho ikiwa ni wivu wa mapenzi.

Akithibisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda  Abwao, amesema limetokea Juni 14,2025, ambapo mwanamke huyo anadaiwa kuwa katika mgogoro na mwenza wake kwa muda, hali iliyofanya kuchukua uamuzi huo.

“Tuna tukio moja la mwanamke kujiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu huko katika kijiji cha Umanda, Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, aliyetambulika kwa jina la Catherine Fito mwenye umri wa miaka 21, ilipofika saa nne usiku siku ya tarehe 14 Mume wa marehemu alifika nyumbani kwake na kumkuta mwanamke huyo anagalagala chini nje  akiwa anatapika na alipumuuliza akajibu amekunywa sumu ya kuulia wadudu.

“Mgonjwa alipatiwa huduma ya kwanza katika zahanati ya Umanda na baada ya hapo akapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Milambo, lakini hawakufanya hivyo ndugu zake wakamchukua kumrudisha nyumbani na ilipofika saa kumi na mbili jioni siku ya tarehe 15 akafariki dunia akiwa nyumbani kwake na chanzo cha kifo hiki ni wivu wa kimapenzi.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...