Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Catherine Fito, mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa Umanda Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, amejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu, huku chanzo cha kifo hicho ikiwa ni wivu wa mapenzi.

Akithibisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda  Abwao, amesema limetokea Juni 14,2025, ambapo mwanamke huyo anadaiwa kuwa katika mgogoro na mwenza wake kwa muda, hali iliyofanya kuchukua uamuzi huo.

“Tuna tukio moja la mwanamke kujiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu huko katika kijiji cha Umanda, Kata ya Kalunde Manispaa ya Tabora, aliyetambulika kwa jina la Catherine Fito mwenye umri wa miaka 21, ilipofika saa nne usiku siku ya tarehe 14 Mume wa marehemu alifika nyumbani kwake na kumkuta mwanamke huyo anagalagala chini nje  akiwa anatapika na alipumuuliza akajibu amekunywa sumu ya kuulia wadudu.

“Mgonjwa alipatiwa huduma ya kwanza katika zahanati ya Umanda na baada ya hapo akapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Milambo, lakini hawakufanya hivyo ndugu zake wakamchukua kumrudisha nyumbani na ilipofika saa kumi na mbili jioni siku ya tarehe 15 akafariki dunia akiwa nyumbani kwake na chanzo cha kifo hiki ni wivu wa kimapenzi.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...