Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi

Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake Hassan Ndonga ‘Tyson Wa Bongo’  hadi  aombe maji ulingoni.

Bokya ameyasema hayo wakati wa mazoezi kuelekea pambano lao la siku ya Boxing On Boxing Day, Desemba 26,2025 House Masaki Jijini Dar es Salaam, usiku ambao Hassan Mwakinyo atazichapa Stanley Eribo kutoka Nigeria.

Ametamba kuwa fedha itampoza na walimtuma hawajamuambia ukweli ni kipigo gani atakakutana nacho, hivyo kumtahadharidha ikiwezekana asipande ulingoni siku hiyo.

“Ninachomuambia Hassan Ndonga, yaani nitakupiga nitakupakua, sina fomula napiga kushoto napiga kulia. Katika mabondia niliocheza nao hakuna hata mmoja Hassan Ndonga amecheza naye,” ametamba Bokya.

Kwa upande mashabiki wa bondia huyo walikuwa wakimsapoti mazoezini hapo, amesema maandalizi anayofanya bondia wao, mpinzani hawezi kufika hata raundi nne za mchezo.

Mabondia wengine watakaopanda ulingini siku hiyo ni Hamadi Furahisha akizichapa dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri, Ally Ngwando na Mussa Makuka, Issa Simba wa Kahama dhidi ya Wilson Phiri Wa Malawi, huku wanawake ni Hidaya Zahoro dhidi ya Leila Macho, Debora Mwenda kuzichapa na Mmalawi Mariam Dick.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...