Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi

Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake Hassan Ndonga ‘Tyson Wa Bongo’  hadi  aombe maji ulingoni.

Bokya ameyasema hayo wakati wa mazoezi kuelekea pambano lao la siku ya Boxing On Boxing Day, Desemba 26,2025 House Masaki Jijini Dar es Salaam, usiku ambao Hassan Mwakinyo atazichapa Stanley Eribo kutoka Nigeria.

Ametamba kuwa fedha itampoza na walimtuma hawajamuambia ukweli ni kipigo gani atakakutana nacho, hivyo kumtahadharidha ikiwezekana asipande ulingoni siku hiyo.

“Ninachomuambia Hassan Ndonga, yaani nitakupiga nitakupakua, sina fomula napiga kushoto napiga kulia. Katika mabondia niliocheza nao hakuna hata mmoja Hassan Ndonga amecheza naye,” ametamba Bokya.

Kwa upande mashabiki wa bondia huyo walikuwa wakimsapoti mazoezini hapo, amesema maandalizi anayofanya bondia wao, mpinzani hawezi kufika hata raundi nne za mchezo.

Mabondia wengine watakaopanda ulingini siku hiyo ni Hamadi Furahisha akizichapa dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri, Ally Ngwando na Mussa Makuka, Issa Simba wa Kahama dhidi ya Wilson Phiri Wa Malawi, huku wanawake ni Hidaya Zahoro dhidi ya Leila Macho, Debora Mwenda kuzichapa na Mmalawi Mariam Dick.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...