Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi

Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake Hassan Ndonga ‘Tyson Wa Bongo’  hadi  aombe maji ulingoni.

Bokya ameyasema hayo wakati wa mazoezi kuelekea pambano lao la siku ya Boxing On Boxing Day, Desemba 26,2025 House Masaki Jijini Dar es Salaam, usiku ambao Hassan Mwakinyo atazichapa Stanley Eribo kutoka Nigeria.

Ametamba kuwa fedha itampoza na walimtuma hawajamuambia ukweli ni kipigo gani atakakutana nacho, hivyo kumtahadharidha ikiwezekana asipande ulingoni siku hiyo.

“Ninachomuambia Hassan Ndonga, yaani nitakupiga nitakupakua, sina fomula napiga kushoto napiga kulia. Katika mabondia niliocheza nao hakuna hata mmoja Hassan Ndonga amecheza naye,” ametamba Bokya.

Kwa upande mashabiki wa bondia huyo walikuwa wakimsapoti mazoezini hapo, amesema maandalizi anayofanya bondia wao, mpinzani hawezi kufika hata raundi nne za mchezo.

Mabondia wengine watakaopanda ulingini siku hiyo ni Hamadi Furahisha akizichapa dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri, Ally Ngwando na Mussa Makuka, Issa Simba wa Kahama dhidi ya Wilson Phiri Wa Malawi, huku wanawake ni Hidaya Zahoro dhidi ya Leila Macho, Debora Mwenda kuzichapa na Mmalawi Mariam Dick.

spot_img

Latest articles

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

Simba yainyuka Fountain Gate mabao 3-0

Na Mwandishi Wetu  SIMBA imechukua alama zote tatu kwa Fountain Gate kufuatia ushindi wa 3-0...

Mahakama yaipa uhuru Chadema, sasa ruksa kufanya siasa

Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA ya Rufani Tanzania leo 15 Aprili 2026, imekiondolea kifungo cha kutofanya...

Rais Mwinyi akagua Mji wa AFCON Fumba

Na Mwandishi WetuRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali...

More like this

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

Simba yainyuka Fountain Gate mabao 3-0

Na Mwandishi Wetu  SIMBA imechukua alama zote tatu kwa Fountain Gate kufuatia ushindi wa 3-0...

Mahakama yaipa uhuru Chadema, sasa ruksa kufanya siasa

Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA ya Rufani Tanzania leo 15 Aprili 2026, imekiondolea kifungo cha kutofanya...