Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu

MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa Jumanne ya Disemba 16, 2025 katika Kijiji cha Ruanda, Mbinga mkoani Ruvuma.

Mhagama ambaye amekuwa Mbunge wa Peramiho kuanzia mwaka 2005, amefariki dunia jana Alhamisi, Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Ratiba ya mazishi yake iliyotolewa usiku wa Alhamisi na uongozi wa Bunge, inaonesha Ijumaa, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Itega, jijini Dodoma.

Jumamosi ya Disemba 13, 2025, mwili wa Jenista utapelekwa Kanisa Katoliki Kiwanja cha Ndege itakapofanyika ibada.

Viongozi mbalimbali watahudhuria kanisani hapo wakiwemo Spika wa Bunge, Mussa Zungu, Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba na Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi.

Baada ya shughuli ya hapo kanisani, mwili wa Jenista utasafirishwa kwenda Songea, Mkoa wa Ruvuma.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...