e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu

WATAALAMU kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wameisifu TANESCO kwa mafanikio makubwa ya matumizi ya teknolojia katika utoaji huduma kwa wateja, hatua iliyochangia kuongeza ufanisi na kuwahudumia wananchi kwa haraka zaidi.

Wakizungumza wakati wa ziara katika Kituo cha miito ya simu (Call Center) Julai 23, 2026, wataalamu hao walieleza kuvutiwa na mifumo ya kidigitali inayotumiwa na TANESCO kupokea, kufuatilia na kutatua changamoto za wateja, ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii kufikisha taarifa na kupokea mrejesho kwa wakati.

Kwa upande wake, Meneja wa Kituo cha Huduma kwa Wateja TANESCO, Shamu Lameck, alisema ziara hiyo ni fursa ya kubadilishana uzoefu na kuonesha hatua ambazo Shirika limefikia katika kutumia teknolojia kuboresha huduma kwa wateja.

Aliongeza kuwa kutambuliwa kwa TANESCO kama kituo cha kujifunzia na taasisi mbalimbali kunathibitisha mafanikio ya juhudi za Shirika katika kuimarisha huduma za kidigitali na kuongeza uzoefu bora kwa wateja.

Ziara ya e-GA ni sehemu ya mwendelezo wa ujio wa taasisi na wadau mbalimbali wanaotembelea Kituo cha Call Center cha TANESCO kujifunza mbinu bora za utoaji huduma kwa wananchi.

spot_img

Latest articles

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

More like this

KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB),...

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...