KAIMU MSAJILI TPRB ASHIRIKI MAFUNZO ELEKEZI YA UONGOZI KWA WATENDAJI WAKUU WA TAASISI, MASHIRIKA YA UMMA NA WAKALA ZA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu

KAIMU Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji (TPRB), TP. Martha Mkupasi, ameshiriki mafunzo elekezi kwa watendaji wakuu wa Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali yanayolenga kuimarisha uongozi wenye matokeo na kuongeza uwajibikaji katika utendaji wa taasisi za umma unaoendana na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

TP. Mkupasi amehudhuria mafunzo hayo yaliyoongozwa na kaulimbiu isemayo “Kutoka Maono Mpaka Matokeo: Kufungamanisha Utekelezaji wa Mashirika ya Umma na DIRA 2050”, yaliyoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Taasisi ya Uongozi, yaliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.

Akizungumza baada ya kushiriki mafunzo hayo ya siku nne, TP. Martha Mkupasi amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwani yamewajengea viongozi hao uwezo wa kuunganisha maono ya kitaifa katika majukumu ya kila siku ndani ya taasisi na yatawasaidia kuandaa mipango inayoakisi utekelezaji malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Amesema wamepata fursa ya kujifunza namna bora ya kusimamia taasisi kwa kuzingatia matokeo, kuandaa mipango, uwajibikaji na ubunifu ikiwa ni njia ya kuwasaidia kuchangia kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwa manufaa ya umma.

spot_img

Latest articles

TAEC YAFANYA UKAGUZI WA MATUMIZI SALAMA YA MIONZI MKOANI LINDI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bwn. Natalis Linuma, amesema...

Msajili wa Hazina aitaka TANROADS kuongeza ufanisi

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, leo, Septemba 18, 2026, ametoa...

TANESCO IMEJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO – MD TWANGE

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limejipanga kukabiliana na...

MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba...

More like this

TAEC YAFANYA UKAGUZI WA MATUMIZI SALAMA YA MIONZI MKOANI LINDI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bwn. Natalis Linuma, amesema...

Msajili wa Hazina aitaka TANROADS kuongeza ufanisi

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, leo, Septemba 18, 2026, ametoa...

TANESCO IMEJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO – MD TWANGE

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limejipanga kukabiliana na...