Na Mwandishi wetu
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania imetangaza uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo utakaofanyika Agosti 16, 2025 jijini Tanga.
Taarifa ya Mwenyekiti wa kamati hiyo, Wakili Kiomoni Kibamba imeeleza kuwa, nafasi zinazogombewa ni Rais wa TFF (nafasi moja) pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji (nafasi sita)

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, gharama za kuchukua fomu kwa nafasi ya Rais ni Sh 500,000 na nafasi za wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Sh 200,000.
Fomu zitaanza kutolewa makao makuu ya TFF na kwenye tovuti ya TFF kuanzia Juni 16-20, 2025.