Ofisi ya Msajili Hazina yalenga kukusanya Sh1 trilioni kama mapato yasiyo ya kodi

Na Mwandishi Wetu

OFISI ya Msajili wa Hazina ina shauku ya kukusanya Sh1 trilioni kama mapato yasiyo ya kodi katika mwaka huu wa fedha wa 2024/25.

Akizungumza katika kikao na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam Jumatatu, Juni 2, 2025, Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu alisema tayari karibia Sh900 bilioni zimekusanywa kutoka taasisi za umma na kampuni ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache zipatazo 200.

“Hadi kufikia sasa (Juni 2, 2025) Ofisi ya Msajili wa Hazina imekusanya karibia Sh900 bilioni kama mapato yasiyo ya kodi na matamanio yetu ni kukusanya Sh1 trilioni katika mwaka wa fedha wa 2024/25,” amesema Mchechu.

Amefafanua kuwa, ikiwa Ofisi hiyo itafanikiwa kukusanya Sh1 trilioni, itakuwa ni ongezeko la asilimia 30.4 ikilinganishwa na mwaka wa fedha uliopita ambapo kiasi cha Sh767 bilioni kilikusanywa.

Ili kuhakikisha Ofisi hiyo inafikia adhima hiyo ya kukusanya Sh1 trilioni, Msajili wa Hazina amezitaka taasisi ambazo bado hazijawasilisha gawio zifanye hivyo ndani ya wiki hii.

“Taasisi zote ambazo bado hazijawasilisha gawio kwa serikali, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, zinapaswa kufanya hivyo ndani ya wiki hii ili ifikapo siku ya Gawio, Juni 10 mwaka huu, asiwepo wa kudaiwa,” amesema Mchechu.

Mchechu amesema ukuaji wa mapato yasiyo ya kodi umetokana na kuimarishwa kwa utaratibu wa ufuatiliaji wa karibu wa gawio na michango katika Mashirika ya umma na matumizi ya Mifumo ya TEHAMA.

“Ofisi imefanikiwa kuunganisha Mfumo wa Mpango na Bajeti (PlanRep) na Mifumo ya ERMS na e-Watumishi pamoja na kufanya maboresho ya Mfumo wa MUSE ambao unawezesha kupata taarifa halisi za matumizi katika Taasisi na Mashirika ya Umma ili kuongeza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za Umma,” amesema Mchechu.

Amesema maboresho hayo sasa yamefanya mifumo kubadilishana taarifa ipasavyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan aliyetaka kuona mifumo inasomana.

spot_img

Latest articles

Tanesco yashinda Tuzo ya uhifadhi wa Mazingira kupitia Mradi wa JNHPP

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya uhifadhi wa...

Dkt. Biteko aweka jiwe la Msingi ujenzi wa Kituo kikubwa cha gesi Afrika Mashariki

📌 Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini 📌 Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa 📌Kampeni ya...

Dkt. Mpango awataka wadau wa Mazingira kuendeleza upandaji miti

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip...

Aliyekuwa Rais wa Zambia, Edgar Lungu afariki dunia

Na Mwandishi wetu Rais  wa  zamani  wa Zambia, Edgar Lungu, amefariki dunia  akiwa na umri wa miaka 65 baada...

More like this

Tanesco yashinda Tuzo ya uhifadhi wa Mazingira kupitia Mradi wa JNHPP

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya uhifadhi wa...

Dkt. Biteko aweka jiwe la Msingi ujenzi wa Kituo kikubwa cha gesi Afrika Mashariki

📌 Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini 📌 Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa 📌Kampeni ya...

Dkt. Mpango awataka wadau wa Mazingira kuendeleza upandaji miti

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip...