Rais wa Malawi aagiza kuondoa majeshi yake DRC

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Malawi, Lazarus Chakwera amemuagiza Kamanda wa Jeshi la nchi hiyo kujiandaa kuondoa Majeshi ya Malawi, kutoka eneo la Mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kulingana na taarifa Televisheni ya Serikali.

Taarifa hiyo ilisema uamuzi wa Rais unalenga kuheshimu tangazo la kusitisha mapigano kati ya pande zinazozana, ingawa uamuzi wa kusitisha mapigano ulikuwa ni mpango wa waasi wa M23, ambao uliibuka baada ya kundi hilo kushambulia Nyabibwe katika Jimbo la Kivu Kusini mwa DRC.

Rais Lazarus Chakwera alikuwa chini ya shinikizo la kuondoa Majeshi ya nchi yake Mashariki mwa DRC, baada ya wanajeshi watatu wa Malawi kuuawa katika mashambulizi ya M23 mjini Goma.

Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Ujumbe wa kulinda amani wa Kusini mwa Afrika uliotumwa na SADC kusaidia mamlaka ya Congo, kukabiliana na makundi yenye silaha katika eneo la mashariki linalokabiliwa na mzozo.

spot_img

Latest articles

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...

Serikali yawataka wakuu taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya kazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewataka wakuu wa taasisi za umma kutengeneza mazingira rafiki ya...

More like this

Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa,...

Maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum UVCCM yamekamilika

Pichani ni Viongozi wa sekretarieti ya Umoja wa Vijana CCM wakikabidhi vifaa mbalimbali wezeshi...

INEC: Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye Uchaguzi Mkuu 2025

Na Tatu Mohamed TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema imeweka mazingira wezeshi...