Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz.

Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya kupoteza mchezo kwa kufungwa ugenini na Silver Strikers bao 1-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa usiku huu, timu itakuwa chini ya Kocha Msaidizi Patrick Mabedi, huku mchakato wa kumtafuta mwingine ukiendelea.

Folz raia wa Ufaransa alijiunga na Wanajangwani hao, Julai, 2025 akitokea klabu ya Olympique Akbou ya Algeria ambako alikuwa Mkurugenzi wa Ufundi.

Kocha Romuald Rakotondrabe kutoka Madagascar anatajwa kuwa ndiye atakayechukua nafasi ya Mfaransa huyo.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...