Rais Samia azitaka Halmashauri kutoa huduma bora kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu

Rais  Dk. Samia Suluhu Hassan, amezitaka Halmashauri kutumia ofisi mpya zinazojengwa katika maeneo yao, kuboresha maeneo ya kazi na kutoa huduma bora na kutakua kwa wananchi

Akizungumza leo Septemba 25,2024 wakati akizindua jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma, amesema ofisi hizo zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Madhumuni ya Serikali kujenga nyumba hizi ni kuleta mazingira mazuri kwa Maafisa wetu wanaofanya kazi ndani ya Halmashauri hizi, wito wangu ni kwamba ofisi hizi zitumike kuondoa kero za wananchi, pili Mkurugenzi Mtendaji na watumishi wote muweze kulitunza jengo hili kama lilivyo leo, kila tukija lionekane hivihivi,” amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo na kuboresha huduma za jamii, hivyo kuwataka watendaji kuweka nguvu katika kusimamia miradi ili yanayowakera wananchi yaondoke.

“Utumishi wetu mimi na nyinyi  kuhudumia wanachi, sisi ni watumishi wa wananchi na sio mabwana wa wananchi, sio watawala wa wananchi, sisi ni watumishi kwa wananchi, ndio maana Serikali inashusha fedha nyingi ili zifanyiwe kazi wananchi hawa waondoshewe shida zao,” amesisitiza.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...