COASCO: Ukaguzi wa vyama vya ushirika waongeza uwazi na kuimarisha imani ya wanachama

Na Tatu Mohamed

Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limesema ukaguzi unaofanywa katika vyama vya ushirika umeendelea kuongeza uwazi, uwajibikaji na kuimarisha imani ya wanachama katika uendeshaji wa vyama hivyo nchini.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COASCO, CPA Jeremiah Mugeta, alisema hayo alipotembelea banda la Wizara ya Kilimo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo taasisi mbalimbali zilizo chini ya wizara hiyo zinaonesha huduma na shughuli zinazotekelezwa katika kuendeleza sekta ya kilimo.

Alisema ushirika una nafasi kubwa katika kukuza kilimo na uchumi wa taifa kwa kuwa unawaunganisha wakulima na kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa pamoja, huku COASCO ikiwa na jukumu la kuhakikisha vyama hivyo vinaendeshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

“Ukaguzi ni muhimu kwa sababu unatoa picha halisi ya mwenendo wa vyama vya ushirika, matumizi ya fedha na kusaidia kutoa ushauri wa namna ya kuimarisha utendaji wa vyama hivyo,” alisema Mugeta.

Alieleza kuwa COASCO imejipanga kuhakikisha vyama vyote vya ushirika vinapata huduma za ukaguzi na ushauri ili viweze kuimarika zaidi na kutoa manufaa kwa wanachama wake.

Amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, shirika hilo litaendelea na mpango wa kufanya ukaguzi wa vyama vya ushirika nchini, huku akiwataka viongozi wa vyama hivyo kuandaa taarifa za fedha kwa wakati ili kurahisisha mchakato wa ukaguzi.

Kwa mujibu wa Mugeta, hali ya uendeshaji wa vyama vya ushirika imeendelea kuimarika ikilinganishwa na miaka iliyopita, ambapo idadi ya vyama vinavyopata hati safi imeongezeka kutoka asilimia nne hadi zaidi ya asilimia 16.

Alisema mafanikio hayo yanaonesha kuwa jitihada za Serikali katika kuimarisha sekta ya ushirika zimeanza kuleta matokeo chanya.

Aidha, Mugeta alisema sekta ya kilimo ina mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania, ikichangia zaidi ya asilimia 26 ya pato la taifa, huku ushirika ukiwa sehemu muhimu ya kuongeza thamani ya mazao na kukuza kipato cha wakulima.

Aliwahimiza wanachama wa vyama vya ushirika kushirikiana na wakaguzi na kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu za uendeshaji ili kuendelea kujenga vyama imara na vyenye tija.

COASCO imeendelea kusisitiza kuwa kupitia ukaguzi na utoaji wa ushauri wa kitaalamu, vyama vya ushirika vitaendelea kuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya kilimo na uchumi wa Tanzania.

spot_img

Latest articles

Ni hofu ya maandamano au ni kutotambua mzizi wa tatizo?

BADO tupo katika mtanziko. Ukisikiliza kwa makini yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii, kwenye vijiwe...

Mbeya City yabaki Ligi Kuu,  kocha akiri kukumbana na changamoto

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Mbeya City imefanikiwa kusalia Ligi kuu ya soka  Tanzania bara...

TOSCI: Mbegu bora ni msingi wa kuongeza tija na kukuza uchumi

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imewahimiza wakulima kutumia...

TPRB YAENDELEA KUTOA HUDUMA SABASABA, YAPOKEA MAOMBI YA USAJILI

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipangomiji (TPRB) imeendelea kutoa huduma...

More like this

Ni hofu ya maandamano au ni kutotambua mzizi wa tatizo?

BADO tupo katika mtanziko. Ukisikiliza kwa makini yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii, kwenye vijiwe...

Mbeya City yabaki Ligi Kuu,  kocha akiri kukumbana na changamoto

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Mbeya City imefanikiwa kusalia Ligi kuu ya soka  Tanzania bara...

TOSCI: Mbegu bora ni msingi wa kuongeza tija na kukuza uchumi

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imewahimiza wakulima kutumia...