Mbeya City yabaki Ligi Kuu,  kocha akiri kukumbana na changamoto

Na Mwandishi Wetu

Klabu ya Mbeya City imefanikiwa kusalia Ligi kuu ya soka  Tanzania bara kufuatia ushindi wa jumla wa 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons kwenye michezo miwili ya mchujo (playoff) wa kusalia Ligi kuu.

Mbeya City iliibuka na ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza kabla ya kutoshana nguvu kwa sare tasa kwenye mchezo wa pili uliopigwa leo Julai 8,2026,  dimba la Sokoine, Mbeya huku Prisons wakielekea kwenye mchujo wa pili dhidi ya timu ya Polisi Tanzania kutoka Championship ili kujinusuru kushuka daraja.

 Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mchezo huo, Kocha wa Mbeya City, Salim Mayanga amesema wamejifunza kutokana na changamoto walizokutana nazo na wanachosubiri ni mabadiliko kwa ajili ya msimu ujao.

 “Timu itafanya marekebisho kwenye maeneo yote yaliyokuwa na udhaifu mkubwa msimu huu. Kutakuwa na ulazima wa kuongeza wachezaji wenye uwezo kwenye maeneo ambayo yalionekana kuwa na mapungufu makubwa,” amesema Mayanga.

 Aidha Mayanga ametoa shukrani zake kwa mashabiki wa Mbeya na uongozi wa timu kwa ushirikiano wao, huku akiahidi kuwa wataendelea kufanya tathmini ya kina kuhusu kiwango cha ushindani wa ligi na jinsi ya kuleta mabadiliko chanya ndani ya kikosi hicho.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...