Chalamila awaalika wakazi wa Dar kujitokeza kwa wingi uzinduzi wa Kituo cha biashara cha EACLC

Na Tatu Mohamed

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewaalika Watanzania na wakazi wa Jiji hilo kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa Kituo Kikubwa cha Biashara na Usafirishaji (EACLC), utaofanyika Agosti 1, 2025 katika eneo la zamani la Stendi Kuu ya Ubungo.

Chalamila amesema uzinduzi huo utafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye atakuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ya kihistoria.

“Nitoe wito kwa wananchi wote, wafanyabiashara waliokwisha chukua maduka, wale wanaotarajia kuchukua, na wote wanaopenda maendeleo ya biashara nchini, wafike kushuhudia tukio hili muhimu. Ni uzinduzi wa kituo ambacho kitabadilisha taswira ya biashara si tu Tanzania, bali Afrika Mashariki kwa ujumla,” amesema Chalamila.

Ameeleza kuwa kituo hicho kikubwa kimejengwa katika eneo ambalo awali lilikuwa Stendi ya Ubungo, baada ya serikali kuhamishia shughuli hizo Mbezi.

“Katika eneo hilo, serikali kupitia Mamlaka ya Uwekezaji kwa kushirikiana na wawekezaji kutoka China, imefanikisha ujenzi wa kituo cha kisasa cha kibiashara.

“EACLC ni mradi wa kimkakati uliogharimu zaidi ya dola milioni 100. Kina maduka zaidi ya 2,000, maghala ya kisasa, sehemu za ofisi, maegesho ya magari, na huduma nyingi nyingine za kibiashara zinazopatikana kwa kukodishwa kwa Watanzania na hata wageni kutoka nje,” alifafanua.

Amesema Kituo hicho kilianza kujengwa Mei 2023 na sasa ujenzi wake umekamilika.

Chalamila amesema ujenzi huo ni ishara ya dhamira ya serikali kuendeleza mazingira ya biashara na uwekezaji nchini, huku akisisitiza kuwa uwekezaji huo haujachukua nafasi ya wafanyabiashara wazawa bali ni mfumo wa ubia unaowanufaisha wote.

Ametoa wito kwa wawekezaji wengine kufika kwenye Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi kupata taarifa sahihi za jinsi ya kuwekeza nchini.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...