Prof. Kabudi: Anayefanya kazi bila ‘Press Card’ anavunja Sheria

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari.

Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika, Julai 14, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Phillip Mpango jijini Arusha.

Amesema Press Card aliyopewa siyo kwa hisani bali ni kutokana na kukidhi vigezo, akiwa amewasilisha vyeti vya taaluma ya Uandishi wa Habari kwenye mfumo wa Bodi, huku akiwasisitiza Waandishi wengine kujisajili katika mfumo wa TAI-HABARI.

Waziri Kabudi amemuhoji Katibu Mtendaji Mstaafu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) ambao ni wenyeji wa Mkutano huo, Kajubi Mukajanga kama ameshajisajili na kupata Press Card, ambapo amekiri kuwa bado lakini atafanya hivyo siku chache zijazo nyaraka zake zikikamilika.

Mkutano wa Mabaraza la Habari Afrika unafanyika kwa mwaka wa pili nchini Tanzania ukitanguliwa na Mkutano wa kwanza uliofanyika Mwaka jana nchini Afrika Kusini.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...