Prof. Kabudi: Anayefanya kazi bila ‘Press Card’ anavunja Sheria

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari.

Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika, Julai 14, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Phillip Mpango jijini Arusha.

Amesema Press Card aliyopewa siyo kwa hisani bali ni kutokana na kukidhi vigezo, akiwa amewasilisha vyeti vya taaluma ya Uandishi wa Habari kwenye mfumo wa Bodi, huku akiwasisitiza Waandishi wengine kujisajili katika mfumo wa TAI-HABARI.

Waziri Kabudi amemuhoji Katibu Mtendaji Mstaafu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) ambao ni wenyeji wa Mkutano huo, Kajubi Mukajanga kama ameshajisajili na kupata Press Card, ambapo amekiri kuwa bado lakini atafanya hivyo siku chache zijazo nyaraka zake zikikamilika.

Mkutano wa Mabaraza la Habari Afrika unafanyika kwa mwaka wa pili nchini Tanzania ukitanguliwa na Mkutano wa kwanza uliofanyika Mwaka jana nchini Afrika Kusini.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...