Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka ili kujenga kanda salama na wenye maendeleo kwa manufaa ya wananchi. 

Ameyasema halo leo Juni 6,2025  wakati akifunga  Mkutano wa 30 wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kutoka nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kupitia Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa nchi wanachama wa SARPCCO katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.

Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi wanachama kuhakikisha utekelezaji wa mikakati hiyo kwa vitendo.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Camillus Wambura, ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa SARPCCO amesema mkutano huo umejikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya ulinzi na usalama katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka.

 IGP Wambura ameongeza kuwa Mkutano huo umejadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto za uhalifu ikiwa ni pamoja na kubadilishana taarifa, kuimarisha uwezo wa kiufundi na kuanzisha operesheni za pamoja.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Sekretarieti ya SADC, Profesa Kula Theletsane, amehimiza umuhimu wa ushirikiano wa kanda katika kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaovuka mipaka.

Amesema wamekubaliana kwa kauli moja kuimarisha ushirikiano wao katika kukabiliana na uhalifu huo na wamejizatiti kuanzisha mikakati ya pamoja itakayowezesha kubadilishana taarifa za kijasusi, kuimarisha mawasiliano kati ya nchi wanachama na kuanzisha operesheni za pamoja.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...