Mawaziri wa Nishati Jumuiya ya SADC kukutana nchini Zimbabwe

📌Masuala ya Umeme, Gesi, Nishati Safi kujadiliwa

Na Mwandishi Wetu

KAMISHNA wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga ameongoza jopo la Wataalam kutoka Wizara ya Nishati katika Kikao cha awali cha Kamati Ndogo ya Nishati ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kilicholenga kujadili maandalizi ya Mkutano wa Pamoja wa Kamati ya Mawaziri wa SADC wanaoshughulikia masuala ya Nishati utakaofanyika nchini Zimbabwe.

Kikao hicho cha awali kimefanyika tarehe 30 Mei 2025 katika Ukumbi wa Wizara ya Nishati jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao.

Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa SADC unatarajia kufanyika nchini Zimbabwe Mei 30 hadi Juni 04, 2025 ukitanguliwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Nishati wa SADC.

Kikao hicho cha Mawaziri kitajadili ajenda mbalimbali ikiwemo hali ya upatikanaji wa nishati ya umeme katika Kanda; Maendeleo ya sekta ndogo ya Mafuta na Gesi, Matumizi ya Nishati Safi na kujadili nafasi na utayari wa Kanda katika kutekeleza Azimo la Dar es Salaam lililotokana na Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Misheni 300.

Washiriki wengine katika kikao hicho kilichofanyika kwa njia ya mtandao wametoka katika nchi zote zilizopo katika Jumuiya ya SADC.

spot_img

Latest articles

e-GA yaimarisha sekta ya kilimo kupitia mifumo ya kidijitali

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (e-GA) imeeleza kuwa inaendelea kushirikiana na Wizara...

WMA YAANZA KUTOA ELIMU YA VIPIMO KATIKA MAONESHO YA NANE NANE

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Vipimo (WMA) umeanza kutoa elimu ya vipimo kwa wakulima,...

TADB yaendelea kuwa nguzo muhimu katika kufadhili mapinduzi ya kilimo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amesema Benki ya Maendeleo ya...

BRELA yatumia Nanenane kuhamasisha urasimishaji wa biashara

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umetoa wito kwa wakulima...

More like this

e-GA yaimarisha sekta ya kilimo kupitia mifumo ya kidijitali

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (e-GA) imeeleza kuwa inaendelea kushirikiana na Wizara...

WMA YAANZA KUTOA ELIMU YA VIPIMO KATIKA MAONESHO YA NANE NANE

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Vipimo (WMA) umeanza kutoa elimu ya vipimo kwa wakulima,...

TADB yaendelea kuwa nguzo muhimu katika kufadhili mapinduzi ya kilimo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amesema Benki ya Maendeleo ya...