Bandari chanzo kingine cha Biashara ya Kaboni

Na Mwandishi Wetu

Hayo yaamelezwa na Bw. Ingvar M. Mathisen, Mkurugenzi mkuu wa Bandari ya Oslo, Norway kwa ujumbe wa Tanzania uliotembelea bandari hiyo hivi karibuni.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Masauni, ulitembelea bandari hiyo kwa lengo la kujifunza namna Bandari ya Oslo inahifadhi mazingira na kuzuia uzalishaji wa gesi joto.

Akizungumza , Mkurugenzi mkuu wa Bandari hiyo Bw. Mathisen ameeleza kuwa Bandari ya Oslo ni bandari mtambuka na haizalishi gesi joto. Bandari ya Oslo ni bandari ya tatu kwa ukubwa duniani kwa kuwa na teknolojia janja ya bahari.

Lengo kuu la bandari hiyo ni kuhakikisha kuwa inapunguza jesi joto kwa 85% ifikapo mwaka 2030.

Serikali hiyo imeazimia kufikia lengo hilo kwa kutumia teknolojia.

Kuanzia mwaka 2018 Bandari ya Oslo, Norway imeacha kupokea na kuendesha meli zake kwa kutumia mafuta, badala yake meli zao iwe za kisafirisha abiria, mizigo au starehe zote zinatumia umeme.


Hivyo kwa vyombo vyote ambavyo havitumii teknolojia hiyo, bandari ya Oslo hutoza ada ya uzalishaji gesi joto-‘ Emission Fees’( inayo jumishwa kwenye mpango wa biashara ya Kaboni).

Tanzania ni nchi ambayo Mashariki yake ina pwani ndefu ya bahari ya Hindi ambayo ina bandari kubwa ya Dar Es Salaam, Mtwara na Tanga aidha kuna bandari ndogo zinazohudumia Lindi, Kilwa Masoko, Mafia, Pangani na Kwale.

Bandari zote hizi hutumia vyombo vya usafirishaji. Hivyo kwa kuwa na teknolojia ya kutambua kila chombo huzalisha kiasi gani cha gesi joto, Mamlaka husika kwa kushirikiana na Kituo cha Ufuatiliaji wa Kaboni – NCMC zinaweza kufanya biashara hiyo kwa kudai ada ya uzalishaji gesi joto.

Kupitia ziara hiyo Tanzania imebainisha fursa mbalimbali za uhifadhi na usimamizi wa Mazingira kupitia Uchumi wa Buluu na Biashara ya Kaboni.

spot_img

Latest articles

JAB YASOGEZA HUDUMA ZA ITHIBATI KARIBU NA WAANDISHI DODOMA

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza kutoa huduma...

Wadau wavutiwa elimu ya vipimo maadhimisho wiki ya utumishi wa umma

Na Mwandishi Wetu WADAU mbalimbali waliotembelea Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika siku ya...

Tanesco yakamilisha miradi ya kuimarisha upatikanaji wa umeme Dodoma

📌 Itanufaisha wilaya za Kongwa,Gairo, Mpwapwa, na Chamwino 📌 Waziri Ndejembi azindua Kituo cha...

Taasisi za Umma Kukabidhi gawio Ikulu Juni 30 Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina imetangaza siku ya Gawio 2026 itafanyika...

More like this

JAB YASOGEZA HUDUMA ZA ITHIBATI KARIBU NA WAANDISHI DODOMA

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza kutoa huduma...

Wadau wavutiwa elimu ya vipimo maadhimisho wiki ya utumishi wa umma

Na Mwandishi Wetu WADAU mbalimbali waliotembelea Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika siku ya...

Tanesco yakamilisha miradi ya kuimarisha upatikanaji wa umeme Dodoma

📌 Itanufaisha wilaya za Kongwa,Gairo, Mpwapwa, na Chamwino 📌 Waziri Ndejembi azindua Kituo cha...