Bandari chanzo kingine cha Biashara ya Kaboni

Na Mwandishi Wetu

Hayo yaamelezwa na Bw. Ingvar M. Mathisen, Mkurugenzi mkuu wa Bandari ya Oslo, Norway kwa ujumbe wa Tanzania uliotembelea bandari hiyo hivi karibuni.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mha. Masauni, ulitembelea bandari hiyo kwa lengo la kujifunza namna Bandari ya Oslo inahifadhi mazingira na kuzuia uzalishaji wa gesi joto.

Akizungumza , Mkurugenzi mkuu wa Bandari hiyo Bw. Mathisen ameeleza kuwa Bandari ya Oslo ni bandari mtambuka na haizalishi gesi joto. Bandari ya Oslo ni bandari ya tatu kwa ukubwa duniani kwa kuwa na teknolojia janja ya bahari.

Lengo kuu la bandari hiyo ni kuhakikisha kuwa inapunguza jesi joto kwa 85% ifikapo mwaka 2030.

Serikali hiyo imeazimia kufikia lengo hilo kwa kutumia teknolojia.

Kuanzia mwaka 2018 Bandari ya Oslo, Norway imeacha kupokea na kuendesha meli zake kwa kutumia mafuta, badala yake meli zao iwe za kisafirisha abiria, mizigo au starehe zote zinatumia umeme.


Hivyo kwa vyombo vyote ambavyo havitumii teknolojia hiyo, bandari ya Oslo hutoza ada ya uzalishaji gesi joto-‘ Emission Fees’( inayo jumishwa kwenye mpango wa biashara ya Kaboni).

Tanzania ni nchi ambayo Mashariki yake ina pwani ndefu ya bahari ya Hindi ambayo ina bandari kubwa ya Dar Es Salaam, Mtwara na Tanga aidha kuna bandari ndogo zinazohudumia Lindi, Kilwa Masoko, Mafia, Pangani na Kwale.

Bandari zote hizi hutumia vyombo vya usafirishaji. Hivyo kwa kuwa na teknolojia ya kutambua kila chombo huzalisha kiasi gani cha gesi joto, Mamlaka husika kwa kushirikiana na Kituo cha Ufuatiliaji wa Kaboni – NCMC zinaweza kufanya biashara hiyo kwa kudai ada ya uzalishaji gesi joto.

Kupitia ziara hiyo Tanzania imebainisha fursa mbalimbali za uhifadhi na usimamizi wa Mazingira kupitia Uchumi wa Buluu na Biashara ya Kaboni.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...