TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika wa michezo ya kubashiri(kubeti) katika mashindano yake yote.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF  waliyotoa leo, Mei 12, 2025 mshirika huyo atashikilia haki hizo kwa kipindi chote cha makubaliano, hivyo yeyote mwenye nia au kuhitaji ‘Odds’ kwa ajili ya mechi ambazo zitakuwa chini ya TFF atalazimika kuwasiliana na mshirika huyo.

“Makubaliano yetu na mshirika huyo yatakuwa ni kwa ajili ya odds tu na si ushirika mwingine na kampuni za michezo ya kubashiri(betting companies) kama udhamini(sponsorship) au ushirikiano,” imesema taarifa hiyo kwa umma.

Taarifa hiyo imesema kuwa utaratibu huo ndio unaotumika katika ligi mbalimbali barani Ulaya, ikieleza kuwa itazinufaisha kimapato klabu mechi zao zitakuwa zimeingia kwenye odds.

“Licha ya malipo yatakayokuwa yanatokana na odds, bado klabu zitaendelea kudhaminiwa na kampuni hizo michezo ya kubashiri, kwani utaratibu huu hauathiri makubaliano ya udhamini kati ya pande hizo.

“Utaratibu wa kumpata mshirika huyo utafanyika kwa njia ya mnada utakaotangazwa  wakati wa utakapowadia,” imesema.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...