Hamza Johari: Tunataka kuwa Champion wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050

Na Mwandishi Wetu

MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeshiriki kikamilifu katika kutoa maoni katika utengenezaji na uandaaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 ili kuhakikisha kuwa Dira hiyo inaakisi masuala yote ya Sekta ya Sheria.

Ameyasema hayo katika mahojiano maalumu na Vyombo vya Habari yaliyofanyika Ofisini kwake, Machi 10, 2025, Mtumba Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Ofisi yake imejipanga kuhakikisha kwamba mambo yote yanayoihusu Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yanatekelezwa ipasavyo ili kuweza kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2050.

“Sisi kama Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali tutahakikisha kwamba tunaoanisha vizuri Sheria zetu tulizonazo na kule tunakotaka kwenda, ni lazima tuwe na legal framework ya kutufikisha,” amesema.

Amesisitiza suala la kufanya maboresho katika Sheria mbalimbali ziweze kuendana na mabadiliko ya Kijamii, Kiuchumi pamoja na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa Sheria.

“Sisi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali tunataka kuwa champion wa kuhakikisha kuwa sheria zetu zote tunazioanisha na Dira ya Taifa ya 2050,” ameongeza.

Katika hatua nyingine Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameongelea suala la ufasiri wa Sheria, ambapo amasema kwakua Sheria mbalimbali zimeweza kutasfiriwa kutoka lugha ya Kingereza kwenda Kiswahili kwakuwa ili ziweze kutumika kwa urahisi na watumiaji.

“Kwa kipindi cha kuanzia Julai hadi Desemba 2024 tumeweza kutafsiri jumla ya Sheria kuu 300 lengo kubwa ikiwa ni kuwarahisishia watumiaji wa Sheria,” amesema.

Sambamba na hilo, Johari amesema kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeweza kukamilisha zoezi la Urekebu wa Sheria, ambapo Sheria mbalimbali zilizorekebishwa zimeweza kufanyiwa Urekebu, hivyo watumiaji wa Sheria watapata Sheria hizi zikiwa zimerekebishwa kwa wepesi zaidi.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...