Watu 37 washikiliwa kwa makosa ya mtandao

Na Mwandishi Wetu

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 37 kwa tuhuma za makosa ya kimtandao ikiwemo kutoa vitisho na kutumia lugha chafu mtandaoni, hatua ambayo imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama wa kidijitali katika Jiji la Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Aprili 27, 2026, watuhumiwa hao wamekamatwa Aprili 20, 2026 katika eneo la Ubungo kufuatia operesheni maalum iliyotegemea taarifa kutoka kwa wananchi na wadau wa usalama, ambapo baadhi yao wamebainika kuwa wafanyakazi wa kampuni zinazotoa huduma za mikopo kwa njia ya mtandao.

Aidha, baadhi ya Watuhumiwa waliotajwa ni pamoja na Renatus Mujwahuzi maarufu Migeyo Mkazi wa Mbezi Beach, Odilia Oswin maarufu Ngunga Mkazi wa Goba Njia Nne pamoja na Theresia Brastius maarufu Kanu Mkazi wa Mtoni Kijichi huku wengine 34 wakiendelea kushikiliwa na kufanyiwa uchunguzi zaidi.

Pamoja na hayo, Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam wamesema wanaendelea na hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa hao, huku wakisisitiza dhamira yao ya kudhibiti vitendo vya kihalifu mtandaoni vinavyoathiri ustawi wa jamii na usalama wa raia, na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za vitendo vya kihalifu ili viweze kufanyiwa kazi kwa haraka na wahusika kufikishwa Mahakamani kwa mujibu wa sheria zilizopo nchini.

spot_img

Latest articles

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...

More like this

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...