Wachezaji volleyball nchini watakiwa kujituma kuwavutia mawakala wa kimataifa


Na Mwandishi Wetu

WACHEZAJI wa mpira wa wavu ‘volleyball’ wanaoshiriki Ligi ya Mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kutumia jukwaa hilo kuonyesha vipaji vyao ili kujiongezea nafasi ya kuonekana na mawakala, timu za ndani na nje ya nchi.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Ligi ya Chama cha Mpira wa Wavu Mkoa wa Dar es Salaam (DAREVA), Joseph Mwaduwa wakati huu ambao ligi hiyo inaendelea.

Mwaduwa amesema ligi hiyo imekuwa daraja muhimu kwa wachezaji wanaotamani kufikia timu za taifa na kupata fursa za kucheza kimataifa.

Amesema wachezaji wanapaswa kujituma na kuonyesha uwezo wao kila wanapopata nafasi ya kucheza kwani mawakala na wadau mbalimbali wa mchezo huo wanafuatilia maendeleo ya wachezaji kupitia mashindano ya ligi.

“Niwaombe wachezaji watumie vizuri nafasi hii ya ligi kuonyesha vipaji vyao. Kupitia ligi wanaweza kuonekana na kupata nafasi ya kuitwa katika timu ya taifa au hata kusajiliwa na klabu za nchi jirani na nyingine za nje ya Tanzania,” amesema.

Ameeleza kuwa ligi ya mwaka huu imekuwa bora kutokana na maandalizi yalifanyika tofauti na mwaka jana.

spot_img

Latest articles

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

📌 Kukamilika kwa njia mpya kutatoa fursa kwa njia ya awali kuendelea kunufaisha wananchi...

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...

More like this

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

📌 Kukamilika kwa njia mpya kutatoa fursa kwa njia ya awali kuendelea kunufaisha wananchi...

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...