Trump: Sina uhakika na uwepo wa amani Israel na Hamas

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hana uhakika na kuwepo kwa amani ya kudumu kati ya Israel na Hamas licha ya kuwa sehemu ya mpango wa kusitisha mapigano uliowezesha kuachiwa kwa mateka ambapo akizungumza kabla ya mkutano wake na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Trump amekiri kuwa hali bado ni tete na haitabiriki.

Netanyahu aliyewasili Washington kwa mazungumzo hayo anakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa washirika wake wenye msimamo mkali wa kisiasa ambao wanataka mashambulizi dhidi ya Hamas yaendelezwe lakini Wakati huo huo Wananchi wa Israel wanamtaka ahakikishe mateka waliosalia wanaachiwa na vita vya miezi 15 vinakoma.

Hata hivyo, Hamas imesisitiza kuwa haitatoa mateka zaidi bila Israel kuondoa Wanajeshi wake kutoka Gaza suala linalozua mgawanyiko ndani ya Serikali ya Netanyahu ambapo Bezalel Smotrich Mshirika wake wa siasa kali ametishia kuiangusha Serikali ikiwa vita dhidi ya Hamas havitaendelea.

Pamoja na hayo, Trump ameibua mpango wa kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza kwenda Misri na Jordan ingawa mataifa hayo yamekataa wazo hilo na Wachambuzi wanaonya kuwa msimamo huo wa Trump unaweza kuhatarisha juhudi za kufanikisha usuluhishi kati ya Israel na Saudi Arabia kwani mazungumzo hayo yanasisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuundwa kwa Taifa huru la Palestina.

spot_img

Latest articles

Sowah, Kante wafungiwa, Aucho naye yumo

Na Winfrida Mtoi NYOTA wa Simba Jonathan Sowah na Allasane Kante wamefungiwa michezo mitano na...

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

More like this

Sowah, Kante wafungiwa, Aucho naye yumo

Na Winfrida Mtoi NYOTA wa Simba Jonathan Sowah na Allasane Kante wamefungiwa michezo mitano na...

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...