Trump: Sina uhakika na uwepo wa amani Israel na Hamas

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hana uhakika na kuwepo kwa amani ya kudumu kati ya Israel na Hamas licha ya kuwa sehemu ya mpango wa kusitisha mapigano uliowezesha kuachiwa kwa mateka ambapo akizungumza kabla ya mkutano wake na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Trump amekiri kuwa hali bado ni tete na haitabiriki.

Netanyahu aliyewasili Washington kwa mazungumzo hayo anakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa washirika wake wenye msimamo mkali wa kisiasa ambao wanataka mashambulizi dhidi ya Hamas yaendelezwe lakini Wakati huo huo Wananchi wa Israel wanamtaka ahakikishe mateka waliosalia wanaachiwa na vita vya miezi 15 vinakoma.

Hata hivyo, Hamas imesisitiza kuwa haitatoa mateka zaidi bila Israel kuondoa Wanajeshi wake kutoka Gaza suala linalozua mgawanyiko ndani ya Serikali ya Netanyahu ambapo Bezalel Smotrich Mshirika wake wa siasa kali ametishia kuiangusha Serikali ikiwa vita dhidi ya Hamas havitaendelea.

Pamoja na hayo, Trump ameibua mpango wa kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza kwenda Misri na Jordan ingawa mataifa hayo yamekataa wazo hilo na Wachambuzi wanaonya kuwa msimamo huo wa Trump unaweza kuhatarisha juhudi za kufanikisha usuluhishi kati ya Israel na Saudi Arabia kwani mazungumzo hayo yanasisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuundwa kwa Taifa huru la Palestina.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande ijitafakari upya

KATIKA dunia tunayoishi sasa suala la uwazi katika kuendesha mambo limekuwa miongoni mwa nguzo...

Msajili wa Hazina azindua Mpango Mkakati wa NMB 2026–2030

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa...

Tanesco yafanya ukaguzi wa Mita kitaalamu kubaini ukweli malalamiko ya umeme kuisha haraka yagundua mita zipo sawa

📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo...

Vijana Dar wakutana kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa Rais Samia, wasifu mchango wake kwa maendeleo ya vijana

Na Mwandishi Wetu VIJANA Jijini Dar es Salaam wameungana kusherehekea siku ya kumbukizi ya...

More like this

Tume ya Jaji Chande ijitafakari upya

KATIKA dunia tunayoishi sasa suala la uwazi katika kuendesha mambo limekuwa miongoni mwa nguzo...

Msajili wa Hazina azindua Mpango Mkakati wa NMB 2026–2030

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa...

Tanesco yafanya ukaguzi wa Mita kitaalamu kubaini ukweli malalamiko ya umeme kuisha haraka yagundua mita zipo sawa

📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo...