Trump: Sina uhakika na uwepo wa amani Israel na Hamas

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hana uhakika na kuwepo kwa amani ya kudumu kati ya Israel na Hamas licha ya kuwa sehemu ya mpango wa kusitisha mapigano uliowezesha kuachiwa kwa mateka ambapo akizungumza kabla ya mkutano wake na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Trump amekiri kuwa hali bado ni tete na haitabiriki.

Netanyahu aliyewasili Washington kwa mazungumzo hayo anakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa washirika wake wenye msimamo mkali wa kisiasa ambao wanataka mashambulizi dhidi ya Hamas yaendelezwe lakini Wakati huo huo Wananchi wa Israel wanamtaka ahakikishe mateka waliosalia wanaachiwa na vita vya miezi 15 vinakoma.

Hata hivyo, Hamas imesisitiza kuwa haitatoa mateka zaidi bila Israel kuondoa Wanajeshi wake kutoka Gaza suala linalozua mgawanyiko ndani ya Serikali ya Netanyahu ambapo Bezalel Smotrich Mshirika wake wa siasa kali ametishia kuiangusha Serikali ikiwa vita dhidi ya Hamas havitaendelea.

Pamoja na hayo, Trump ameibua mpango wa kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza kwenda Misri na Jordan ingawa mataifa hayo yamekataa wazo hilo na Wachambuzi wanaonya kuwa msimamo huo wa Trump unaweza kuhatarisha juhudi za kufanikisha usuluhishi kati ya Israel na Saudi Arabia kwani mazungumzo hayo yanasisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuundwa kwa Taifa huru la Palestina.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...