Vita ya kusaka tiketi ya China 2026 yanoga, Waogeleaji 200 wachuana vikali

Na Winfrida Mtoi

IKIWA ni siku ya pili ya Mashindano ya Taifa ya mchezo wa kuogelea,   waogeleaji  wa klabu mbalimbali wameendelea kuchuana vikali kufatuta rekodi mpya, huku  rekodi zikiendelea kuvunjwa.

Miongoni mwa waogeleaji waliofanikiwa kuvunja rekodi katika mashindano hayo ni Crissa Dillip  kutoka klabu ya Tallis aliyevunja rekodi ya mita 100 free style kwa wasichana.

Mashindano hayo yanayofanyika katika bwawa la kuogelea la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika(IST), Masaki, jijini Dar es Salaam, yanashirikisha waogeleaji 200 kutoka klabu 16.

Bila kujali hali ya hewa ya mvua katika mashindano hayo, ushindani  ni mkali kutokana na uwezo wa washiriki, huku kila mmoja akitamani kuvunja rekodi.

Akizungumzia mashindano hayo, Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo wa Kuogelea  Tanzania (TSA), David Mwansyoge amesema  mashindano yamezingatia vigezo vya hali ya juu kwa sababu yanatumika  kufuzu Mashindano ya Dunia ya Kuogelea (World Aquatics Short Course Championship) yatakayofanyika nchini China Desemba 2026.

“Jana tulianza na umbali mrefu mita 800, tukiamini kwamba umbali mrefu ni eneo ambalo tunaweza kufanya vizuri zaidi katika muda mfupi.Tumeona rekodi zikivunjwa na tunategemea rekodi nyingi kuvunjwa kwa kuwa ushindani ni mkubwa,” ameeleza Mwansyoge.

Kwa upande wake Crissa akielezea  ubora wake  anasema ni kutokana na sapoti anayopa kuanzia kwa wazazi wake, huku akiwataka wasichana kujitokeza katika mchezo huo.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...