Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu

Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza kila kitu ndani ya dakika 90 katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho dhidi ya TMA  Stars utakaopigwa kesho kwenye dimba la KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 10, Okello amesema wapinzani wao hawana cha kupoteza lakini upande wa Yanga wakipoteza itakuwa ni habari kubwa zaidi, hivyo kuwataka wachezaji wenzake kuzingatia maelekezo ya mwalimu.

“Nina matumaini makubwa kama tutaendelea na morali ya mchezo uliopita basi tutapata ushindi wa kishindo. Wachezaji tunapaswa kuwa watulivu uwanjani na kufuata maelekezo ya waalimu wetu. Ukifanya kosa moja tu kwenye mchezo wa mtoano inaweza kubadilish historia. Hii sio ligi. Ninawahakikishia wananchi kuwa tutamaliza kila kitu ndani ya dakika 90”

Hata hivyo ameeleza kuwa hawabezi wapinzani wao, kwani mpira unahitaji kuwa na heshima kwa kila mpinzani, bali ni wajibu wa kila mchezaji wa kuzingatia malengo yao na kutumia nguvu ile ile wanayotumia katika Ligi Kuu.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...