SACP Mahanga: Ulinzi viwanjani unahitaji ujasili

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Polisi Jamii Kamisheni ya Polisi Zanzibar, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Jonas Mahanga amesema suala la ulinzi na usalama katika viwanja vya michezo linahitaji moyo na ujasiri pamoja na uadilifu ili kuweza kufikia malengo ya kuimarisha sekta za michezo.

Ameyasema hayo wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu ya maofisa wa ulinzi na usalama viwanjani, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa New Amaan Complex ambayo yaliandaliwa na Shirikisho la Soka Zanzibar (ZFF).

Amesema siku zote katika kufikia mafanikio ni lazima kuwe na watu waliojitolea kwa hali na mali na wenye uchungu wa kutaka kufikia mafanikio husika.

Ameeleza kuwa kazi ambayo wameisomea ni ngumu katika mazingira yaliyowazunguka, hivyo inahitaji ujasiri wa hali ya juu na kuwa na uadilifu kwa maslahi ya michezo.

“Hii ni kazi ngumu wala musione masihara na ukiichukulia urahisi hatuwezi kufika mbali ni lazima tuwe makini na tuache muhali”, amesema SACP Mahanga.

Naye Mkufunzi wa mafunzo hayo, Ramadhan Manyama amesema washiriki hao walipata mafunzo hayo kwa muda wa siku tatu na watakabidhiwa vyeti vya kuhitimu mafunzo hayo.

Amesema walijifunza mada mbalimbali kuhusiana na masuala ya ulinzi na anaamini wameyaelewa na watakuwa na mabadiliko viwanjani.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Zanzibar, Issa Kassim Ali amesema baada ya mafunzo hayo ana imani kuwa watashirikiana katika masuala yao mbalimbali viwanjani.

Naye Mkuu wa Operesheni na Mafunzo Mkoa wa Kusini Pemba, ASP Hassan Khamis Juma, amesema
elimu waliyoipata wataenda kuifanyia kazi na watakuwa mabalozi kwa wengine ambao hawajapata mafunzo hayo hasa kisiwani Pemba.

spot_img

Latest articles

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...

‘Uandishi wa kidijitali ndiyo mpango mzima’

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya Media Brains ikishirikiana na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Msajili wa Hazina ateta na uongozi wa kampuni ya Barrick

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi...

TUNATAMANI KUWA MABALOZI WA VIPIMO – WANAFUNZI MWANZA

Na WMA - Mwanza WANAFUNZI kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba...

More like this

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...

‘Uandishi wa kidijitali ndiyo mpango mzima’

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya Media Brains ikishirikiana na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Msajili wa Hazina ateta na uongozi wa kampuni ya Barrick

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi...