Rais Samia azitaka Halmashauri kutoa huduma bora kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu

Rais  Dk. Samia Suluhu Hassan, amezitaka Halmashauri kutumia ofisi mpya zinazojengwa katika maeneo yao, kuboresha maeneo ya kazi na kutoa huduma bora na kutakua kwa wananchi

Akizungumza leo Septemba 25,2024 wakati akizindua jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma, amesema ofisi hizo zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Madhumuni ya Serikali kujenga nyumba hizi ni kuleta mazingira mazuri kwa Maafisa wetu wanaofanya kazi ndani ya Halmashauri hizi, wito wangu ni kwamba ofisi hizi zitumike kuondoa kero za wananchi, pili Mkurugenzi Mtendaji na watumishi wote muweze kulitunza jengo hili kama lilivyo leo, kila tukija lionekane hivihivi,” amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo na kuboresha huduma za jamii, hivyo kuwataka watendaji kuweka nguvu katika kusimamia miradi ili yanayowakera wananchi yaondoke.

“Utumishi wetu mimi na nyinyi  kuhudumia wanachi, sisi ni watumishi wa wananchi na sio mabwana wa wananchi, sio watawala wa wananchi, sisi ni watumishi kwa wananchi, ndio maana Serikali inashusha fedha nyingi ili zifanyiwe kazi wananchi hawa waondoshewe shida zao,” amesisitiza.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...