Lugalo yang’ara  shindano la gofu

Na Winfrida Mtoi

Klabu ya Lugalo imeng’ara katika shindano la gofu la  Vodacom Lugalo Open 2024 baada ya mchezaji wa klabu hiyo, Prosper Emmanuel kuibuka mshindi wa jumla wa shindano hilo kwa gross 225.

Mshindi wa pili ni Samweli Kileo akishinda kwa gross 226, watatu Isika Daud gross 229 wote wakitokea katika klabu hiyo, huku mshindi wa kwanza kwa wachezaji wa kulipwa akiwa ni Nuru Morel kutoka Arusha Gymkana kwa gross 147.

Shindano hilo la siku tatu lilihusisha  zaidi ya wachezaji 200 kutoka katika klabu mbalimbali kwa kushikisha vijana, wanawake na watu wazima.

Akizungumza wakati wa kufunga shindano hilo, Waziri wa  Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro ameipongeza klabu ya Lugalo kwa kuwa chachu ya kuendeleza mchezo huo kutokana na kuandaa mashindano mbalimbali na uwepo wa miundombinu bora inayoruhusu mchezo huo kuchezwa muda wowote.

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akipiga mpira katika shindano la gofu kwenye viwanja vya Klabu ya Gofu Lugalo. 

“Nawapongeza sana  Lugalo Golf Klabu, imekuwa ni klabu ambayo inazingatia ubora na viwango, ukifika Lugalo unahisi wewe kweli ni mchezaji, kila kitu kinakuwa  kipo katika ubora unaotakiwa,” amesema.

Aidha Dk. Ndumbaro ameeleza kuwa mustakabari wa mchezo huo upo kwa vijana na wizara yake imepeleka wazo serikalini na limekubaliwa ambapo kuanzia mwakani mchezo wa gofu utachezwa kwenye mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

spot_img

Latest articles

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

More like this

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...