Lugalo yang’ara  shindano la gofu

Na Winfrida Mtoi

Klabu ya Lugalo imeng’ara katika shindano la gofu la  Vodacom Lugalo Open 2024 baada ya mchezaji wa klabu hiyo, Prosper Emmanuel kuibuka mshindi wa jumla wa shindano hilo kwa gross 225.

Mshindi wa pili ni Samweli Kileo akishinda kwa gross 226, watatu Isika Daud gross 229 wote wakitokea katika klabu hiyo, huku mshindi wa kwanza kwa wachezaji wa kulipwa akiwa ni Nuru Morel kutoka Arusha Gymkana kwa gross 147.

Shindano hilo la siku tatu lilihusisha  zaidi ya wachezaji 200 kutoka katika klabu mbalimbali kwa kushikisha vijana, wanawake na watu wazima.

Akizungumza wakati wa kufunga shindano hilo, Waziri wa  Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro ameipongeza klabu ya Lugalo kwa kuwa chachu ya kuendeleza mchezo huo kutokana na kuandaa mashindano mbalimbali na uwepo wa miundombinu bora inayoruhusu mchezo huo kuchezwa muda wowote.

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akipiga mpira katika shindano la gofu kwenye viwanja vya Klabu ya Gofu Lugalo. 

“Nawapongeza sana  Lugalo Golf Klabu, imekuwa ni klabu ambayo inazingatia ubora na viwango, ukifika Lugalo unahisi wewe kweli ni mchezaji, kila kitu kinakuwa  kipo katika ubora unaotakiwa,” amesema.

Aidha Dk. Ndumbaro ameeleza kuwa mustakabari wa mchezo huo upo kwa vijana na wizara yake imepeleka wazo serikalini na limekubaliwa ambapo kuanzia mwakani mchezo wa gofu utachezwa kwenye mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...