Lugalo yang’ara  shindano la gofu

Na Winfrida Mtoi

Klabu ya Lugalo imeng’ara katika shindano la gofu la  Vodacom Lugalo Open 2024 baada ya mchezaji wa klabu hiyo, Prosper Emmanuel kuibuka mshindi wa jumla wa shindano hilo kwa gross 225.

Mshindi wa pili ni Samweli Kileo akishinda kwa gross 226, watatu Isika Daud gross 229 wote wakitokea katika klabu hiyo, huku mshindi wa kwanza kwa wachezaji wa kulipwa akiwa ni Nuru Morel kutoka Arusha Gymkana kwa gross 147.

Shindano hilo la siku tatu lilihusisha  zaidi ya wachezaji 200 kutoka katika klabu mbalimbali kwa kushikisha vijana, wanawake na watu wazima.

Akizungumza wakati wa kufunga shindano hilo, Waziri wa  Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro ameipongeza klabu ya Lugalo kwa kuwa chachu ya kuendeleza mchezo huo kutokana na kuandaa mashindano mbalimbali na uwepo wa miundombinu bora inayoruhusu mchezo huo kuchezwa muda wowote.

Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akipiga mpira katika shindano la gofu kwenye viwanja vya Klabu ya Gofu Lugalo. 

“Nawapongeza sana  Lugalo Golf Klabu, imekuwa ni klabu ambayo inazingatia ubora na viwango, ukifika Lugalo unahisi wewe kweli ni mchezaji, kila kitu kinakuwa  kipo katika ubora unaotakiwa,” amesema.

Aidha Dk. Ndumbaro ameeleza kuwa mustakabari wa mchezo huo upo kwa vijana na wizara yake imepeleka wazo serikalini na limekubaliwa ambapo kuanzia mwakani mchezo wa gofu utachezwa kwenye mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

spot_img

Latest articles

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...

Matendo ya Polisi ni hujuma dhidi ya utawala bora, demokrasia

MFUMO wa uchumi wa soko huru una kanuni zake. Miongoni mwake ni kuruhusu ushindani....

More like this

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...