Twaha Kiduku atamba yupo fiti kumkabili mhindi

Na Winfrida Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Twaha Kiduku leo Aprili 3,2024 amewaongoza mabondia wenzake mkoani Morogoro kupima afya kuelekea pambano lake dhidi ya Hapreet Sight kutoka India.

Pambano hilo la Kimataifa lisilokuwa la ubingwa lililopewa jina la ‘Hatukimbii Hatuogopi’ linatarajia kupigwa siku ya Idd Pili kwenye ukumbi wa Tanzanite, mkoani Morogoro.

Akizungumzia maandalizi yake, Kiduku amesema amekamilisha kwa asilimia kubwa na yupo tayari kuliwakilisha vizuri Taifa kwa kuibuka na ushindi.

“Mimi pamoja na timu yangu tuko vizuri kiafya na kila kitu, naamini siwezi kuwaangusha Watanzania. Hakuna ugomvi rahisi, siku zote ugomvi ni ugomvi kikubwa ni kujiandaa na kumheshimu mpinzani,” amesema Kiduku.

Mara ya mwisho Kiduku alipanda ulingoni Desemba mwaka jana na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhindi ya Mganda, Mohammed Sebyala, jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mratibu wa Habari wa Peak Time ambao ni waandaaji wa pambano hilo, Victor Denis amesema kwa sasa kilichobaki ni mashabiki kuona burudani ya masumbwi kutokana na kila bondia kuwa fiti.

Mabondia wengine watakaozichapa siku hiyo ni Karim Mandonga dhidi ya Mada Maugo,Jamali Kunoga wa Marogoro kuchapana na Mrisho Mzezele wa Mbagala Dar es Salaam na mapambano mengine mengi.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...