Uokoaji waendelea kutafuta watu 20 walioporomoka na daraja la Francis Scott Key Marekani

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Timu za kutafuta na kuokoa zinawatafuta karibu watu 20 ambao hawajulikani walipoa baada ya daraja kubwa kuporomoka katika mji wa Baltimore, Maryland Marekani.

Video ya simu ilionyesha sehemu kadhaa za daraja hilo la Francis Scott Key likianguka kwenye Mto Patapsco baada ya meli ya kontena yenye bendera ya Singapore inayoitwa Dali kugonga nguzo ya Daraja hilo Jumanne alfajiri.

Maafisa wa usalama waasema magari kadhaa yalikuwa kwenye daraja wakati ajali hiyo ilipotokea.

Maafisa wa dharura wa Baltimore wanasema wafanyakazi wa utafutaji na uokoaji wanatafuta takriban watu 20 wanaoaminika kuwa ndani ya maji.

Wasimamizi wa meli ya Dali, Synergy Marine Corp, walitoa taarifa wakisema kuwa meli hiyo iligonga nguzo moja ya daraja hilo na kwamba wafanyakazi wake wote wakiwemo manahodha wawili waliokuwemo wamepatikana na hakuna taarifa zozote za majeruhi

spot_img

Latest articles

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....

Kukataa mgombea binafsi ni kukumbatia utumwa

HISTORIA inashuhudia kwamba wapo watumwa walikataa kuwa huru kwa sababu waliamini kwamba pamoja na...

More like this

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....