Uokoaji waendelea kutafuta watu 20 walioporomoka na daraja la Francis Scott Key Marekani

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Timu za kutafuta na kuokoa zinawatafuta karibu watu 20 ambao hawajulikani walipoa baada ya daraja kubwa kuporomoka katika mji wa Baltimore, Maryland Marekani.

Video ya simu ilionyesha sehemu kadhaa za daraja hilo la Francis Scott Key likianguka kwenye Mto Patapsco baada ya meli ya kontena yenye bendera ya Singapore inayoitwa Dali kugonga nguzo ya Daraja hilo Jumanne alfajiri.

Maafisa wa usalama waasema magari kadhaa yalikuwa kwenye daraja wakati ajali hiyo ilipotokea.

Maafisa wa dharura wa Baltimore wanasema wafanyakazi wa utafutaji na uokoaji wanatafuta takriban watu 20 wanaoaminika kuwa ndani ya maji.

Wasimamizi wa meli ya Dali, Synergy Marine Corp, walitoa taarifa wakisema kuwa meli hiyo iligonga nguzo moja ya daraja hilo na kwamba wafanyakazi wake wote wakiwemo manahodha wawili waliokuwemo wamepatikana na hakuna taarifa zozote za majeruhi

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...