Tano za Yanga zamng’oa kocha Simba

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

UONGOZI wa klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa kikosi hicho, Robertinho Oliveira kwa kuvunja mkataba wake wa miaka miwili aliotumikia kwa kipindi cha miezi 10.

Kocha huyo anaondoshwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya kufungwa na watani zao Yanga mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Jumapili Novemba 5, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho raia wa Brazil, alijiunga na Simba Januari 3, 2023 akitokea Vipers SC ya Uganda na ameiongoza Simba katika michezo zaidi ya 25, ya Ligi Kuu Tanzania Bata na Kimataifa.

Katika Ligi Kuu tangu ametua nchini, amecheza mechi 18, akipoteza moja pekee dhidi ya Yanga huku akitoka sare mbili, huku akiipa Simba taji la Ngao ya Jamii alilotwaa msimu huu baada ya Wanamsimbazi hao kulikosa kwa misimu miwili mfululizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba, pia imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

“Katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola. Tayari mchakato wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi  punde,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

More like this

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...