Tano za Yanga zamng’oa kocha Simba

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

UONGOZI wa klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa kikosi hicho, Robertinho Oliveira kwa kuvunja mkataba wake wa miaka miwili aliotumikia kwa kipindi cha miezi 10.

Kocha huyo anaondoshwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya kufungwa na watani zao Yanga mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Jumapili Novemba 5, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho raia wa Brazil, alijiunga na Simba Januari 3, 2023 akitokea Vipers SC ya Uganda na ameiongoza Simba katika michezo zaidi ya 25, ya Ligi Kuu Tanzania Bata na Kimataifa.

Katika Ligi Kuu tangu ametua nchini, amecheza mechi 18, akipoteza moja pekee dhidi ya Yanga huku akitoka sare mbili, huku akiipa Simba taji la Ngao ya Jamii alilotwaa msimu huu baada ya Wanamsimbazi hao kulikosa kwa misimu miwili mfululizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba, pia imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

“Katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola. Tayari mchakato wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi  punde,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Kilo 101.2 za Mirungi ndani ya Basi la Abood, watano mbaroni

Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata...

Wakurugenzi Media Brains waapishwa kuwa Majaji tuzo za EJAT

Na Mwandishi Wetu WAKURUGENZI wa Kampuni ya Media Brains wameapishwa wameteuliwa na Baraza la Habari...

CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya...

Mchezaji auawa na majambazi nchini Ghana

MCHEZAJI wa soka nchini Ghana, Dominic Frimpong, ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya...

More like this

DCEA yakamata Kilo 101.2 za Mirungi ndani ya Basi la Abood, watano mbaroni

Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata...

Wakurugenzi Media Brains waapishwa kuwa Majaji tuzo za EJAT

Na Mwandishi Wetu WAKURUGENZI wa Kampuni ya Media Brains wameapishwa wameteuliwa na Baraza la Habari...

CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya...