Tano za Yanga zamng’oa kocha Simba

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

UONGOZI wa klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa kikosi hicho, Robertinho Oliveira kwa kuvunja mkataba wake wa miaka miwili aliotumikia kwa kipindi cha miezi 10.

Kocha huyo anaondoshwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya kufungwa na watani zao Yanga mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Jumapili Novemba 5, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho raia wa Brazil, alijiunga na Simba Januari 3, 2023 akitokea Vipers SC ya Uganda na ameiongoza Simba katika michezo zaidi ya 25, ya Ligi Kuu Tanzania Bata na Kimataifa.

Katika Ligi Kuu tangu ametua nchini, amecheza mechi 18, akipoteza moja pekee dhidi ya Yanga huku akitoka sare mbili, huku akiipa Simba taji la Ngao ya Jamii alilotwaa msimu huu baada ya Wanamsimbazi hao kulikosa kwa misimu miwili mfululizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba, pia imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

“Katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola. Tayari mchakato wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi  punde,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

More like this

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...