Tano za Yanga zamng’oa kocha Simba

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

UONGOZI wa klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa kikosi hicho, Robertinho Oliveira kwa kuvunja mkataba wake wa miaka miwili aliotumikia kwa kipindi cha miezi 10.

Kocha huyo anaondoshwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya kufungwa na watani zao Yanga mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Jumapili Novemba 5, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho raia wa Brazil, alijiunga na Simba Januari 3, 2023 akitokea Vipers SC ya Uganda na ameiongoza Simba katika michezo zaidi ya 25, ya Ligi Kuu Tanzania Bata na Kimataifa.

Katika Ligi Kuu tangu ametua nchini, amecheza mechi 18, akipoteza moja pekee dhidi ya Yanga huku akitoka sare mbili, huku akiipa Simba taji la Ngao ya Jamii alilotwaa msimu huu baada ya Wanamsimbazi hao kulikosa kwa misimu miwili mfululizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba, pia imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

“Katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola. Tayari mchakato wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi  punde,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Tumeepuka balaa jingine, uadilifu uongoze tiba machungu ya MO29

JUMANNE wiki hii Watanzania walisherehekea siku ya uhuru wa Tanganyika wengi wakiwa majumbani kwao....

Aweso aridhishwa na wingi wa maji Ruvu Juu, aipa Dawasa jukumu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa maji, Jumaa Aweso amekagua na kujiridhisha na wingi wa...

Prof. Mkenda: Serikali imeendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali...

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

More like this

Tumeepuka balaa jingine, uadilifu uongoze tiba machungu ya MO29

JUMANNE wiki hii Watanzania walisherehekea siku ya uhuru wa Tanganyika wengi wakiwa majumbani kwao....

Aweso aridhishwa na wingi wa maji Ruvu Juu, aipa Dawasa jukumu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa maji, Jumaa Aweso amekagua na kujiridhisha na wingi wa...

Prof. Mkenda: Serikali imeendelea kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali...