Tanzania kuvuna matrilioni kutokana na kaboni

Serikali inatarajia kupata wastani wa shilingi trilioni 2.4 kutokana na biashara ya kaboni ambazo zitachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo amesema bungeni Dodoma kuwa kufikia Desemba 31, 2023 Serikali ilikuwa imekwishapokea maombi 35 ya miradi mbalimbali ya biashara hiyo.

“Katika miaka ya hivi karibuni kumeibuka soko huria la biashara ya kaboni ikijumuisha misitu ya asili na ya kupanda na imeanza kushamiri hapa nchini na kuonesha inaweza kuchangia kwenye pato la taifa,” amesema Dkt. Jafo.

Waziri huyo alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Buhigwe Kavejuru Felix aliyetaka kujua biashara ya kaboni katika misitu ya asili na ya kupanda imechangia kiasi gani pato la taifa tangu iingie nchini.

Waziri Jafo amesema katika kipindi cha mwaka 2018-22 fedha zilizopokelewa kupitia miradi inayotekelezwa kwenye halmashauri mbalimbali hapa nchini inafikia shilingi bilioni 32.

Kuhusu mkakati wa utoaji elimu ya biashara hiyo, Dkt. Jafo amesema Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEM pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii imefanya mkutano na wakuu wa mikoa na wilaya kupeleka ujumbe.

Amesema Tanzania pia imetumia fursa ya ushiriki katika Mkutano wa 28 Mabadiliko ya Tabianchi uliofanyika Dubai, Falme za Kiarabu kutangaza biashara hiyo.

spot_img

Latest articles

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...

Mpina ashinda kesi, ruksa kugombea Urais

Na Mwandishi Wetu Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba...

More like this

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...