Na Mwandishi Wetu
MWAMUZI wa Tanzania wa mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu, Shaban Msangi ameteuliwa kuwa miongoni mwa waamuzi watatu watakaochezesha mechi za Kombe la Dunia kwa watu wenye ulemavu nchini Mexico, Novemba, 2026.
Hii ni mara ya pili kwa mwamuzi huyo kuchezesha Kombe la Dunia, mara ya kwanza alichezesha fainali za mwaka 2022 zilizofanyika Uturuki.
Pamoja na kuwa mwamuzi, Msangi pia ni Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa Watu Wenye Ulemavu Tanzania (TAFF).


