Kampuni ya Media Brains yawapa mbinu za kidigitali waandishi wa habari Iringa

Na Mwandishi Wetu, Iringa

KAMPUNI ya Media Brains kwa kushirikiana na Taasisi ya Konrad Adenauer Stiftung (KAS) imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoa wa Iringa kuhusu uandishi wa habari za kidijitali.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoeanza leo Juni 2, 2026, katika Hoteli ya Sunset, Manispaa ya Iringa, yanalenga kuwaongezea uwezo waandishi wa habari katika kuandaa, kuchakata na kusambaza habari kwa haraka huku wakizingatia misingi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Media Brain, Jesse Kwayu, amesema maendeleo ya sayansi na teknolojia pamoja na mabadiliko ya jamii, hususan vijana ambao wamejikita zaidi katika matumizi ya mitandao ya kijamii, yanawalazimu waandishi wa habari kuendana na mabadiliko hayo.

Ameeleza kuwa matumizi ya majukwaa ya kidijitali yanatoa fursa kwa waandishi wa habari kuwafikia watu wengi zaidi kwa wakati mfupi, hivyo ni muhimu kwao kuongeza ujuzi wa kutumia teknolojia hizo kwa ufanisi bila kuathiri ubora na uaminifu wa habari wanazozitoa.

“Wekezeni kwenye elimu, jifunzeni zaidi. Fanyeni uhakiki wa habari zenu, fanyeni ‘fact checking’ na zaidi, kuweni weledi. Fuateni maadili ya uandishi wa habari,” amesisitiza Kwayu.

Kwa upande wake Meneja Mradi kutoka Konrad Adenauer Stiftung, Damas Nderumaki, amesema ushirikiano wao na Media Brains ni kuhakikisha wanawanoa waandishi wa habari nchini kuhusu habari za kidigitali.

Katika mafunzo hayo washiriki watajifunza mbinu mbalimbali za uandishi wa habari za kidijitali, matumizi ya mitandao ya kijamii katika utoaji wa habari, pamoja na namna ya kukabiliana na changamoto zinazoibuka katika mazingira ya habari ya kisasa.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...