Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi

BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha vijana wa timu ya Serengeti Boys kufika fainali ya AFCON – U17 na kiwango walichoonesha ni fursa ya kwenda kucheza soka la kulipwa katika mataifa makubwa.

Serengeti Boys inatarajia kushuka dimbani kesho kuchuana na Senegar katika mchezo wa fainali wa michuano hiyo katika Uwanja wa Moulay Hassan, Rabat nchini Morocco.

Kibabage ambaye alikuwa miongoni mwa wachezaji waliunda kikosi cha Serengeti Boys iliyofanya vizuri mwaka 2016, ametoa kauli hiyo leo Juni 1, 2026, akiwapongeza vijana hao kwa kuandika historia ya pekee.

Amesema ni jambo la kupongeza kwa sababu Tanzania haijawahi kucheza fainali hizo, akiamini Serengeti Boys ina uwezo wa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo kutokana na kiwango walichoonesha katika michezo yote.

“Kwanza tunawapongeza kwa hatua walitofikia, ni jambo la kihistoria na kesho wanakwenda kukamilisha historia. Ni moja jambo kubwa sana kwa nchi yetu Tanzania, haijawahi kutokea hususani kwa timu za vijana kufika hatua hii”, amebainisha.

spot_img

Latest articles

Wachezaji volleyball nchini watakiwa kujituma kuwavutia mawakala wa kimataifa

Na Mwandishi Wetu WACHEZAJI wa mpira wa wavu 'volleyball' wanaoshiriki Ligi ya Mkoa wa Dar...

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...

More like this

Wachezaji volleyball nchini watakiwa kujituma kuwavutia mawakala wa kimataifa

Na Mwandishi Wetu WACHEZAJI wa mpira wa wavu 'volleyball' wanaoshiriki Ligi ya Mkoa wa Dar...

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...