Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi

BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha vijana wa timu ya Serengeti Boys kufika fainali ya AFCON – U17 na kiwango walichoonesha ni fursa ya kwenda kucheza soka la kulipwa katika mataifa makubwa.

Serengeti Boys inatarajia kushuka dimbani kesho kuchuana na Senegar katika mchezo wa fainali wa michuano hiyo katika Uwanja wa Moulay Hassan, Rabat nchini Morocco.

Kibabage ambaye alikuwa miongoni mwa wachezaji waliunda kikosi cha Serengeti Boys iliyofanya vizuri mwaka 2016, ametoa kauli hiyo leo Juni 1, 2026, akiwapongeza vijana hao kwa kuandika historia ya pekee.

Amesema ni jambo la kupongeza kwa sababu Tanzania haijawahi kucheza fainali hizo, akiamini Serengeti Boys ina uwezo wa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo kutokana na kiwango walichoonesha katika michezo yote.

“Kwanza tunawapongeza kwa hatua walitofikia, ni jambo la kihistoria na kesho wanakwenda kukamilisha historia. Ni moja jambo kubwa sana kwa nchi yetu Tanzania, haijawahi kutokea hususani kwa timu za vijana kufika hatua hii”, amebainisha.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...