Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi

BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha vijana wa timu ya Serengeti Boys kufika fainali ya AFCON – U17 na kiwango walichoonesha ni fursa ya kwenda kucheza soka la kulipwa katika mataifa makubwa.

Serengeti Boys inatarajia kushuka dimbani kesho kuchuana na Senegar katika mchezo wa fainali wa michuano hiyo katika Uwanja wa Moulay Hassan, Rabat nchini Morocco.

Kibabage ambaye alikuwa miongoni mwa wachezaji waliunda kikosi cha Serengeti Boys iliyofanya vizuri mwaka 2016, ametoa kauli hiyo leo Juni 1, 2026, akiwapongeza vijana hao kwa kuandika historia ya pekee.

Amesema ni jambo la kupongeza kwa sababu Tanzania haijawahi kucheza fainali hizo, akiamini Serengeti Boys ina uwezo wa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo kutokana na kiwango walichoonesha katika michezo yote.

“Kwanza tunawapongeza kwa hatua walitofikia, ni jambo la kihistoria na kesho wanakwenda kukamilisha historia. Ni moja jambo kubwa sana kwa nchi yetu Tanzania, haijawahi kutokea hususani kwa timu za vijana kufika hatua hii”, amebainisha.

spot_img

Latest articles

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

📌 Kukamilika kwa njia mpya kutatoa fursa kwa njia ya awali kuendelea kunufaisha wananchi...

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...

More like this

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

📌 Kukamilika kwa njia mpya kutatoa fursa kwa njia ya awali kuendelea kunufaisha wananchi...

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...