TCRA:Elimu usalama wa mtandao inahitajika

Na Esther Mnyika

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema elimu kuhusu usalama wa mtandao inahitajika ili kudhibiti uhalifu wa mtandao.

Hayo yamebainishwa leo Februari 2, 2024 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu TCRA, Dk. Jabir Bakari wakati akifungua semina ya wadau wa masuala ya mtandao wa intaneti katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni .

Amesema kuna haja ya kuwadhibiti wanaotumia mitandao vibaya kwa kufanya matukio ya utapeli kuiba taarifa binafsi za watumiaji wengine kwa lengo la kujinufaisha wenyewe na kuleta matatizo kwa wengine.

“Pamoja na faida za mitandao bado ipo haja kwa wahalifu wa mtandao kudhibitiwa na kupewa elimu ya kutoka kwenye kundi hili la uhalifu na kuwaelimisha wengine kuhusu usalama wa mitandao.

“Pamoja na faida nyingi zitokanazo na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) bado tunaowajibu wa kuendelea kuelimishana kwani kuna baadhi ya watumiaji wanatumia fursa hiyo vibaya kwa kufanya uhalifu, hivyo tunawajibu wa kuwadhibiti,”amesema Dk. Bakari.

Amesema kwa mujibu wa taarifa ya robo ya mwaka hadi Desemba mwaka jana imeonesha kuwa watumiaji wa intaneti Tanzania wamefikia milioni 35.8 huku idadi za simu janja zenye uwezo wa kutumia intaneti ni millioni 19.8.

“Dhana za maendeleo ya teknolojia ya kidigiti kila mmoja ananafasi muhimu ya kuhakikisha anga la mtandao ni salama kwa kuzingatia matumizi sahihi na salama na kuleta tija kwa kila mtu, binafsi pamoja na jamii,”ameongeza.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki katika semina hiyo Dk. Macca Abdalla ambaye ni mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Madirisha Women Cooperative Sector amesema mtandao umemrahisishia matumizi mbalimbali ya teknolojia

Amesema bado baadhi ya wanawake wanaohitaji kupata elimu zaidi ya mtandao ili waweze kujikwamua kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...