TCRA:Elimu usalama wa mtandao inahitajika

Na Esther Mnyika

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema elimu kuhusu usalama wa mtandao inahitajika ili kudhibiti uhalifu wa mtandao.

Hayo yamebainishwa leo Februari 2, 2024 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu TCRA, Dk. Jabir Bakari wakati akifungua semina ya wadau wa masuala ya mtandao wa intaneti katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni .

Amesema kuna haja ya kuwadhibiti wanaotumia mitandao vibaya kwa kufanya matukio ya utapeli kuiba taarifa binafsi za watumiaji wengine kwa lengo la kujinufaisha wenyewe na kuleta matatizo kwa wengine.

“Pamoja na faida za mitandao bado ipo haja kwa wahalifu wa mtandao kudhibitiwa na kupewa elimu ya kutoka kwenye kundi hili la uhalifu na kuwaelimisha wengine kuhusu usalama wa mitandao.

“Pamoja na faida nyingi zitokanazo na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) bado tunaowajibu wa kuendelea kuelimishana kwani kuna baadhi ya watumiaji wanatumia fursa hiyo vibaya kwa kufanya uhalifu, hivyo tunawajibu wa kuwadhibiti,”amesema Dk. Bakari.

Amesema kwa mujibu wa taarifa ya robo ya mwaka hadi Desemba mwaka jana imeonesha kuwa watumiaji wa intaneti Tanzania wamefikia milioni 35.8 huku idadi za simu janja zenye uwezo wa kutumia intaneti ni millioni 19.8.

“Dhana za maendeleo ya teknolojia ya kidigiti kila mmoja ananafasi muhimu ya kuhakikisha anga la mtandao ni salama kwa kuzingatia matumizi sahihi na salama na kuleta tija kwa kila mtu, binafsi pamoja na jamii,”ameongeza.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki katika semina hiyo Dk. Macca Abdalla ambaye ni mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Madirisha Women Cooperative Sector amesema mtandao umemrahisishia matumizi mbalimbali ya teknolojia

Amesema bado baadhi ya wanawake wanaohitaji kupata elimu zaidi ya mtandao ili waweze kujikwamua kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...