Na Mwandishi Wetu
KIUNGO Khalid Aucho amesimamishwa kwa miezi mitatu na klabu yake ya Singida Black Stars kwa kosa la utovu wa nidhamu na utoro kazini.
Klabu hiyo pia imemsimamisha kipa Amas Obasogie kwa kipindi cha miezi mitatu ili kuruhusu uchunguzi wa tuhuma zinazohusiana na upangaji wa matokeo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu hiyo leo Februari 27,2026, uongozi wa klabu kupitia Kamati ya Nidhamu imesema imechukua hatua za kinidhamu, huu ikiwataka wachezaji kuzingatia nidhamu na uwajibikaji.
“Klabu inawakumbusha wachezaji na watumishi wake wote kuzingatia nidhamu, uwajibikaji na heshima kwa klabu,” imesema taarifa hiyo.


