Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) kwenye kilele cha Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika jijini Dodoma.

Mhe. Balozi Dkt. Nchimbi ametembelea banda la hilo leo Juni 5, 2026 ambapo amepata nafasi ya kuelezwa miradi mbalimbali inayotekelezwa na shirika hilo ikiwemo matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme pamoja na utunzaji wa mazingira kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme.

Akitoa maelezo kwa Mhe.Balozi Dkt.Nchimbi Mkuu wa Kitengo cha Mazingira Wizara ya Nishati Emmilian Nyanda ameeleza kuwa TANESCO imekuwa ikifanya jitihada kubwa za kutoa elimu ya umuhimu wa Nishati Safi ya kupikia kwa Umeme kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kwenye suala la utunzaji wa Mazingira.

Maonesho ya mwaka ya mazingira 2026 yalikuwa na kauli mbiu isemayo Dira 2050, Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.

spot_img

Latest articles

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

Tunazidi kujisokota kwenye mtego, au tunajinasua?

TAIFA limechafukwa. Kuchafukwa huku ni kutokana na kile ambacho maseneta wawili wa Marekani, Jeanne...

Ibenge aongezewa mkataba Azam FC

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Azam imemuongezea mkataba kocha wake, Florent Ibenge, akiendelea kusalia katika...

More like this

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

Tunazidi kujisokota kwenye mtego, au tunajinasua?

TAIFA limechafukwa. Kuchafukwa huku ni kutokana na kile ambacho maseneta wawili wa Marekani, Jeanne...