Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu

Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa kushiriki Mashindano ya vilabu kwa nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika kuanzia kesho Juni 6 hadi 7, 2026 katika bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), Masaki jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya mashindano hayo, Mkurugenzi wa Elimu na Maendeleo wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), Jeremiah Keema amesema mashindano hayo yatashirikisha jumla ya vilabu 25 kutoka nchi nne ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda na Zambia.

Keema amesema mashindano hayo yanalenga kuwapa waogeleaji chipukizi nafasi ya kuonesha vipaji vyao, kujenga uzoefu wa ushindani wa kimataifa na kuimarisha mahusiano ya michezo kati ya nchi zinazoshiriki.

Aidha, amebainisha kuwa mashindano hayo ni sehemu ya juhudi za kuendeleza mchezo wa kuogelea kwa vijana na kuandaa kizazi cha waogeleaji watakaoiwakilisha vyema Tanzania katika mashindano ya ngazi mbalimbali siku zijazo.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...