Simba yataka Polisi iwashughulikie waliomkashfu bosi

Na Mwandishi Wetu

KLABU ya Simba imeliandikia barua Jeshi la Polisi  ili kuwachukulia hatua za kisheria wanachama na mashabiki wa klabu hiyo  waliohusika na mkutano wa kutoa kashfa na maneno yasio ya staha kwa mwekezaji wao Mohamed Dewji (Mo).

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Klabu hiyo, Bodi ya Wakurugenzi ya Simba imesikitishwa na vitendo hivyo na kutaka wote waliohusika au kula njama za kuandaa mkutano huo  kufikishwa katika vyombo vya dola kwa makosa ya jinai.

“Bodi inasisitisha kuwa haitabariki wala kuvumilia mtu yoyote anayeharibu taswira ya klabu kwa namna yoyote ile,” imesema taarifa hiyo.

Aidha uongozi wa Simba, umetoa onyo kwa baadhi ya wanachama na mashabiki wa klabu hiyo wanaotumia nembo rasmi ya klabu bila kupata ruhusa ya moja kwa moja kutoka kwa ngazi za juu za klabu hiyo.

Umetoa wito kwa wanachama na mashabiki kuzingatia taratibu rasmi za klabu na kushirikiana kwa pamoja katika kuendeleza heshima na hadhi ya klabu.

spot_img

Latest articles

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

Simba yainyuka Fountain Gate mabao 3-0

Na Mwandishi Wetu  SIMBA imechukua alama zote tatu kwa Fountain Gate kufuatia ushindi wa 3-0...

More like this

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...