Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O dhidi ya mpinzani wake Stanley Eribo kutoka Nigeria, baada ya kumaliza pambano katika raundi mbili.

Pambano hilo limemalizika usiku huu katika ukumbi wa Warehouse Masaki, jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia pambano hilo, Mwakinyo amesema imekuwa rahisi kwake kumshinda mpinzani wake kutokana na mazoezi anayofanya bila kujali ana mchezo au hana.

Amesema ubora wake haushuki hata akikaa muda mrefu bila kucheza kwa kuwa ameweka heshima katika mazoezi na anaamini ndiyo mhimili wa kazi yake.

Katika pambano lingine Mtanzania Hamadi Furahisha ameibuka mshindi kwa pointi dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri katika pambano la raundi 10, huku Hassan Ndonga akimchapa Ismail Boyka.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...