Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu

Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa huru, huku mfanyabiashara wa vipodozi Jenifer Jovin (26) maarufu Niffer na Mika Lucas Chavala kurudishwa rumande.

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) amewafutia kesi hiyo ya uchunguzi namba 26388/ 2025 chini ya kifungu namba 92(1) cha Sheria ya Makosa ya Jinai, Sura ya 20 ilivyofanya marejeo mwaka 2023.

Uamuzi wa kuwafutia kesi hiyo kwa washtakiwa 20, umetolewa leo Jumanne, Novemba 25, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Aaron Lyamuya, baada ya Wakili wa Ssrikali, Titus Aron kuieleza Mahakaka hiyo kuwa DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa 20 kati ya washtakiwa 22 wanakabiliwa na kesi hiyo.

Washtakiwa hao walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Novemba 7, 2025. Kuachiwa huru kwa baadhi ya watuhumiwa kumekuja kutokana na  kauli ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwamba wale waliofuata mkumbo wakati wa vuguvugu za siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 iangaliwe namna ya kuachiwa.

spot_img

Latest articles

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

More like this

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...