Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi

Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijjni Dar es Salaam.

Matokeo hayo yamewafanya mashabiki wa timu hiyo waliojitokeza kwa wingi kuondoka kwa unyonge uwanjani wakiwa hawaamini kilichotokea.

Wikiendi ijayo Simba itakuwa ugenini nchini Mali kuikabili Stade Malien ambayo jana ilitoka suluhu na Esperance ya Tunisia.


Wawakilishi wengine wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC wameanza vibaya hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa kufungwa ugenini mabao 2-0 na AS Maniema ya DR Congo.

Kati ya wawakilishi wanne wa Tanzania katika michuano hiyo ya CAF yaani Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la. Shirikisho, Yanga pekee ndio imeanza vizuri kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FAR Rabat ya Morocco, wakati Singida Bs ikipoteza ugenini kwa kufungwa 2-0 na CR Belouizdad

spot_img

Latest articles

Matendo ya Polisi ni hujuma dhidi ya utawala bora, demokrasia

MFUMO wa uchumi wa soko huru una kanuni zake. Miongoni mwake ni kuruhusu ushindani....

Dkt. Mataragio: Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wanaoficha mafuta

Na Tatu Mohamed SERIKALI imetoa onyo kali kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na vitendo vya kuficha...

Lukuvi afariki dunia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye...

Mgodi wa kihistoria wa niobium kujengwa Mbeya

Na Mwandishi Mbeya TANZANIA imepiga hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na Marekani baada...

More like this

Matendo ya Polisi ni hujuma dhidi ya utawala bora, demokrasia

MFUMO wa uchumi wa soko huru una kanuni zake. Miongoni mwake ni kuruhusu ushindani....

Dkt. Mataragio: Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wanaoficha mafuta

Na Tatu Mohamed SERIKALI imetoa onyo kali kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na vitendo vya kuficha...

Lukuvi afariki dunia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye...